Home » » MFUKO WA FIDIA KWA WAFANYAKAZI, WCF WAENDELEA NA KAMPENI YA KUELIMISHA MADAKTARI KUHUSU FIDIA KWA WAFANYAKAZI WAPATAPO MADHARA KATIKA KAZI

MFUKO WA FIDIA KWA WAFANYAKAZI, WCF WAENDELEA NA KAMPENI YA KUELIMISHA MADAKTARI KUHUSU FIDIA KWA WAFANYAKAZI WAPATAPO MADHARA KATIKA KAZI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 


Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi Bw. Emmanuel Humba, (kulia),  akimkaribisha Naibu Waziri wa Kazi Mhe. Anthony Mavunde alipowasilili kufungua mafunzo kwa Madaktari yanayohusu ajali na maginjwa yanayosababishwa na kazi Jijini Arusha Leo. Katikati ni Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi Bw. Masha Mshomba


NA K-VIS MEDIA/Khalfan Said
Mfuko wa Fidia Kwa Wafanyakazi, (WCF), umeendelea na kampeni yake ya kutoa mafunzo kwa madaktari ili kujenga uelewa wa kufanya tathmini ya  ajali na magonjwa ayapatayo mfanyakazi yanayotokana na kazi safari hii ikihusisha madaktari kutoka mikoa mitano ya ambayo ni Arusha Tanga, Manyara, Kilimanjaro na Singida.
Mafunzo hayo yaliyofunguliwa leo Mei 30, 2016 na Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Watu Wenye Ulemavu, Bw. Anthony Mavunde, huko jijini Arusha, ni muendelezo wa mafunzo mengine kama hayo yaliyotolewa wiki mbili zilizopita jijini Dar es Salaam, ambapo madaktari kutoka mikoa ya Dares Salaam, Pwani, Morogoro, Dodoma, lindi na mtwara walihudhuria.
WCF imechukua hatua hiyo ili kujiandaa na UTOAJI WA Mafao kwa mara ya kwanza tangu uanzishwe ifikapo Julai mwaka huu wa 2016.

Mgeni Rasmi Mhe. Anthony Mavunde (MB), Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Watu Wenye Ulemavu, akisisitiza jambo wakati alipokuwa akifungua Mafunzo kwa Madaktari kujenga uelewa wa kufanya tathmini ya  Ajali na Magonjwa ayapatayomfanyakazi yanayotokana na Kazi Jijini Arusha leo Mei 30, 2016
 Mkurugenzi Mkuu wa WCF, Bw. Masha Mshomba akitoa maelezo ya utangulizi na mipango mbalimbali ambayo Mfuko umejiwekea kwa mujibu wa sheria ili kuhudumia wadau wakuu ambao ni wafanyakazi katika sekta ya umma na binafsi
 Baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo wakinakili kilichokuwa kikizungumzwa kwenye mafunzo hayo
 Mwenyekiti wa Bodiya Wadhamini ya WCF, Bw. Emmanuel Humba, akitoa hotuba ya kumkaribisha mgeni rasmi
Mgeni rasmi Bw. Anthony Mavunde, akizungumza na waandishi wa habari ili kufafanua alichozungumza wakati akifungua mafunzo hayo

0 comments:

 
Supported byBlogs za Mikoa
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa