Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com
Home » » Serikali yaboresha Sekta ya hali ya hewa na kufikia ya kiwango cha kimataifa.

Serikali yaboresha Sekta ya hali ya hewa na kufikia ya kiwango cha kimataifa.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

 
Na Anitha Jonas – MAELEZO.
 
“Wahenga wanasema penye nia pana njia na haja ya mja hunena, muungwana ni vitendo.” Hatimae Serikali imetimiza ndoto zake za kuwa na kituo bora chenye kutoa  taarifa za uhakika zinazohusu masuala ya hali ya hewa katika kiwango cha Kimataifa.
 
Serikali imeweza kufanikisha hili kwa kupitia taasisi yake ya Mamlaka ya Hali ya Hewa (TMA) ambapo mpaka sasa imefanikiwa kuboresha huduma hizo kwa asilimia 80. Haya ni mafanikio makubwa kutokana na ukweli kwamba kufahamu habari za hali ya hewa kunasaidia sana kupanga shughuli za kiuchumi na maendeleo.

Hilo limejidhihirisha hivi karibuni katika taarifa ya tahadhari kuwepo kwa mvua zitakazo ambatana na upepo kutokana na kuimarika kwa ukanda wa mvua sambamba na uwepo wa kimbunga Fantala katika Bahari ya Hindi.
 
Taarifa hiyo ilitolewa na Mkurugenzi Mkuu Mamlaka ya Hali ya Hewa, Dkt. Agness Kijazi na kusema mvua hizo zinatarajiwa kunyesha kuanzia Aprili 13-16,2016 ambapo kutakuwa na mvua kubwa inayozidi milimita 50 ndani ya saa 24. na hili limetokea kama lilivyotabiriwa. Wenye kuchukua tahadhari wamesha hivyo na kuepuka madhara yatokanayo na mafuriko. Waliohama baadhi ya sehemu za mabondeni, walishukuru baada ya kuona makazi yao ya awali yakifunikwa kabisa na maji.
 
Mvua hizo zilikuwa zikiathiri mkoa wa Tanga, Dar es Salaam, Pwani,Morogoro pamoja na visiwa vya unguja na Pemba.
 
Kuthibitisha kuwa kituo hicho kinatoa taarifa za uhakika ni pale ambapo mwaka jana Dkt. Agness Kijazi alitangaza kuwepo na mvua za EL-NINO kuanzia mwanzoni mwa mwezi Septemba–Desemba 2015. Hii ilithibitika baada kushuhudia kuwepo kwa mvua hizo katika maeneo mbali mbali ya nchi ambapo        mvua hizo zilisababisha mafuriko na uharibifu wa miundombinu,makazi na mazao ya wakulima.

Utabiri huo wa kuaminika unatokana na TMA kuboresha mtandao wa vituo na usimikaji wa mitambo ya hali ya hewa pamoja na kuongeza idadi ya vituo vya hali ya hewa ambapo vituo vitatu vyenye mitambo ya kisasa vimejengwa katika maeneo mbalimbali ikiwemo Kilwa Masoko- Lindi, Mpanda-Katavi na Songwe.Vituo hivi vimechangia kuongeza upatikanaji wa takwimu na taarifa za hali ya hewa kwa shughuli mbalimbali za kijamii na kiuchumi nchini.
 
Kwa sasaSerikali kupitia TMA imeanzisha kituo cha kupimia hali ya hewa na Kilimo kiitwacho Agromet Station hukoMatangutuani Pemba na hivyo kuongeza idadi ya vituo vya kutoa huduma za hali ya hewa katika sekta ya Kilimo na kufikia vituo 15 nchini,hivyo kuongeza ubora wa taarifa zinazotolewa.

Kwa upande wa taarifa za anga ya juu Mamlaka imeimarisha huduma za Usafiri wa Anga kwa kuboresha mtambo wa kupima hali ya hewa katika anga za juu (Modernization of Upper Air System) katika kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere Dar es Salaam (JNIA) pamoja na kufufua kituo cha kupima taarifa za anga ya juu kilichopoTabora.
 
TMAkatika kuimarisha huduma za utoaji wa  taarifa za hali ya hewa nchini  imefanikiwa kuanzisha vituo 11 vya kupima hali ya hewa nchini katika kipindi 2010-2015 ambapo vituo hivyo vimewekwa maeneo mbalimbali ikiwemo Moshi(Kisangesangeni,Maweni,UparonaMasila,Lindi,Nachingwea,Tunduru,Msata (Bagamoyo),Nzega (Tabora),Makete (Njombe) na Chanika (Dar es Salaam).

Ili kufikia viwango vya kimataifa kwa masuala ya upimaji wa hali ya hewaa Dkt.Kijazi anabainishakuwa Mamlaka imenunua Mitambo Mitano (5) ya Kisasa ya kupima hali ya hewa inayojiendesha yenyewe (Automatic Weather Station) kupitia mradi wa Mobile Weather Alert. Mitambo hiyo  imekwishafungwa katika sehemu mbalimbali hapa nchini,pamoja na
mtambo wa kuchambua data (Computer Cluster) ambao umefungwa katika  JNIA na hivyo kusaidia kuboresha utabiri wa hali ya hewa hususani kwa watumiaji waZiwa Nyasa na Victoria.
                                                        
 “Kuna Mitambo mingine 16 ya kupima hali ya hewa nchini ambayo imenunuliwa kupitia mradi wa (CIRDA) chini ya udhamini wa Shirika la Maendeleo (UNDP) ambapo taratibu za kufunga mitambo hiyo zimekamilika kwa asilimia kubwa”aliongeza Dkt.Kijazi.

Mbali na hayo Mamlaka kwa sasa hutoa huduma za hali ya hewa katika Bandari ya Zanzibar pamoja na ZiwaVictoria, Ziwa Nyasa na Ziwa Tanganyika – Kigoma na kuboreshwa kwa huduma hizo katika maeneo hayo kumeifanya  Mamlakakuweza kutoa utabiriwa hali ya hewa katika Maziwa  yote nchini tofauti na ilivyokuwa awali kwamba utabiri wa hali ya hewa ulikuwa ukifanyika katika bahari tu.

Katika uboreshaji huu, Mamlaka imeanzisha vituo viwili vya Rada za hali ya hewa katika eneo la Bangulo,Dar es Salaam tangu Aprili 2011 pamoja na kituo cha  Kiseke – Mwanza ambacho kimekamlika hivi karibuni. Vituo hivi vimekuwa mchango mkubwa katika kutoa taarifa za uhakika kwa wakati. Rada za hali ya hewa ni muhimu katika uboreshaji wa utabiri wa hali ya hewa hususani katika utabiriwa hali mbaya ya hewa.
 
Pamoja na hayo Mamlaka inamiliki mtambo unaotumika kuhakiki vifaa vya kupimia mkandamizo wa hewa (Pressure Calibration Unit) ambao umefungwa katika karakana ya Mamlaka ya Hali ya hewa iliyopo Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Dar es Salaam eneo la UwanjaMdogo (Terminal 1).

Aidha,Mamlaka ya Hali ya Hewa kwa kushirikiana na Idara ya Mazingira, Ofisi ya Makamu wa Rais pamoja na vyuo vikuu nchini inafanya tafiti mbalimbali za mabadiliko ya hali ya hewa kama vile Mradi wa Climate Change Impact Adaptation and Mitigation-(CCIAM) ambapo pia tafiti juu ya elimu ya asili ya utabiri wa hali ya hewa (Indigenous knowledge) zinafanyika.
 
Mbali na hayoSerikali kupitia TMA imeboresha Chuo cha Hali ya Hewa Kigoma kwa kuongeza idadi ya walimu, vitendea kazi na kuboresha miundombinu ya Chuo na kuhakikisha kinapata usajili wa NACTE.Chuo hicho hutoa Mafunzo ya Diploma katika fani ya hali ya hewa (Meteorological Technician Senior Level Course).

Hata hivyo Mamlaka kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam imekuwa ikitoa Shahada ya kwanza ya Sayansi ya Hali ya Hewa (BSc, Meteorology) kuanzia mwaka wa masomo 2013/2014.

TMA kwa kushirikiana na Kampuni za simu za mkononi zaVodacom na Tigo imekuwa ikitoa tarifa za huduma za hali ya hewa kupitia ujumbe mfupi wa maandishi wa simu za mkononi (sms) na lengo likiwa ni kurahisisha upatikanaji wa tarifa za hali ya hewa kwa umma.
 
Mbali na hayo naye Bi. Merry Kadaya mkazi wa Kilosa,Mkoa wa Morogoro alipohojiwa kuhusu taarifa za hali ya hewa zinazotolewa na TMA alisema anaipongeza Mamlaka kwa kazi wanayoifanya  kwani  kwa sasa wamekuwa wananatoa taarifa za uhakika zisizona na shaka,pia ameiomba serikali kujiandaa pale wanapopata taarifa hizo ili kuwaweza kuwaokoa wananchi.


Halikadhalika,takwimu za hali ya hewa zina umuhimu katika shughuli mbalimbali kama katika tafiti za Mafuta na Gesi (Oil and gas exploration) pamoja naMipango ya Maendeleo ya Kiuchumi na Kijamii. Mkulima anategemea sana kujua hali ya hewa ili kilimo chake kiwe na tija. Utabiri wa hali ya hewa ni wa muhimu sana pia kwenye suala zima la usafiri, ujenzi wa miundombinu kama barabara, reli, viwanja vya ndege na madaraja. Hivyo uboreshaji na ongezeko la vituo vya kisasa vya hali ya hewa ni hatua moja kubwa katika maendeleo ya Taifa.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa