Home » » Wakonta: Binti aliyepania kusaidia watu wenye mahitaji maalum(Waliopooza).

Wakonta: Binti aliyepania kusaidia watu wenye mahitaji maalum(Waliopooza).


Na: Frank Shija, MAELEZO

Wakonta msichana aliyepata ajali ya gari amewaomba wa samaria wema kujitolea kumsaidia ili aweze kutimiza ndoto zake za kuwasaidia watu wengine wenye matatizo yanayofanana na tatizo lake kupitia uandishi wa Filamu na kuanzisha Taasisi itakayosaidia kutoa mahitaji maalum kwa watu hao.
Ombi hilo limetolewa na Msichana huyo Wakonta Mapunda alipokuwa akiongea na waandishi wa habari katika ukumbi wa Idara ya Habari - MAELEZO leo Jijini Dar es Salaam.
Wakonta amesema kuwa kutokana na changamoto alizokumbana nazo baada ya kupata ajali ikiwa ni pamoja na kutumia ulimi kuandika amejikuta akiwa muandishi wa Filamu hivyo anakusudia kutumia ujuzi huo kusaidia watu wenye matatizo kama yake.
Amesema kuwa lengo lake kubwa ni kuwa muandishi wa Filamu zitakazo waunganisha jamii,kutia moyo na faraja zitakazo kuwa kiungo muhimu cha watu wenye uhitaji maalum.
Ameongeza kuwa katika kuhakikisha anatimiza malengo yake hayo amemekusudia kuanzisha Tasisi itakayokuwa ikitoa misaada kwa na kuwawezesha watu wenye matatizo kama yake katika kuwapatia mitaji na huduma za kijamii.
Aidha ametoa wito kwa wadau mbalimbali wenye uwezo kifedha kuweza kushirikiana naye katika kuanzisha Taasisi hiyo ili hatimaye watu wenye uhitaji maalum wapate mahali pa kupatia misaada na huduma zao.
Akizungumzia changamoto anazokabiliana nazo Wakonta amesema kuwa suala la gharama za matibabu limekuwa kikwazo kikubwa kwake ambapo mpaka sasa anatakiwa kufanyiwa kipimo cha CT Scan MRI katika hospitali ya Taifa Muhimbili ambacho kina gharama kubwa.
Ameomba wasamaria wema kumsaidi ili aweze kufanikisha kupata huduma hiyo ambapo alitaja njia ya kumfikishia msaada huo kuwa ni Benki ya CCRDB Akaunti namba, Jina la Akaunti Wakonta Kapunda, Akaunti na. 0152292436800, M-PESA 0755836896, Airtel Money 0683886446 na TIGO PESA 0656771529
Kwa upande wake Baba mzazi wa binti huyo, Brazilio Kapunda  amesema kuwa wao kama familia wanamuunga mkono mtoto wao katika kufika ndoto zake za kuwa muuandishi mahiri wa Miswada ya Filamu na kuanzisha Taasisi itakayo kuwa inawasidia watu wenye mahitaji kama yake.
Aliongeza kuwa kwao ilikuwa ni mtihani mkubwa kwakuwa tukio hilo lilitokea pasipo kutarajiwa
Awali akitoa historia ya mkasa wake uliompelekea kukutwa na matatizo hayo alisema ilikuwa ni tarehe 3 Februari 2012 siku ambayo walikuwa na mahafali ya kumaliza kidato cha sita katika shule ya Sekondari ya Wasichana ya Korogwe, ndipo ajali mbaya iliwakuta wakiwa wanafunzi tisa baada ya mwenzao mmoja kuingia ndani ya gari la ndugu yake aliyekuja kumtembela na ghafla gari hilo lilianza kurudi nyuma kwa kasi kubwa ndipo walipokutwa na majanga hayo.
“Hapo ndio ilipokua mwanzo wa safari yangu ambayo sijawahi hata kuifikiria kwani nilivunjika uti wa mgongo na kupooza kutoka mabegani mpaka miguuni. Nilifanyiwa operation Muhimbili bila mafanikio.Nimekuwa mtu wa kukaa na kulala tu,muda mwingi nimekuwa nautumia kuangalia Filamu ndipo alipojikuta ametamani kuwa muandishi wa miswada ya Filamu”
Wakonta amesema kuwa baada ya kuwa anaangalia Filamu kwa muda mrefu alijikuta navutiwa na uigizaji wa msanii mmoja katika Filamu ya kihindi inayojulikana kwa jina la “Like Stars from Heaven”ambapo mhusika mkuu alikuwa mtoto mwenye matatizo ya ubongo alikumbana changamoto kadhaa hatimaye alifanikiwa kuonyesha kuwa kuna kitu anaweza kufanya kwa manufaa ya jamii.

0 comments:

 
Supported byBlogs za Mikoa
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa