Waziri wa Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu Mhe.
Jenista Mhagama anatarajiwa kufungua maonesho ya wajasiliamali
yatofanyika Septemba 26 katika viwanja vya Mlimani City ambayo
yameandaliwa na Taasisi ya Ujasiriamali na ushindani Tanzania(TEEC) kwa
kushirikiana na Baraza la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC) pamoja na Taasisi ya Sekta Binafsi nchini (TPSF) ili kukuza uchumi wa nchi.
Akizungumza
na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam Katibu Mtendaji wa NEEC
Bi. Beng’i Issa amesema kuwa maonesho hayo yatalenga kuwawezesha
wananchi kuwa wabunifu katika sekta ya biashara ili kupiga hatua kufikia
uchumi wa kati.
“Maonesho
ambayo yatafanyika kesho ni kwa ajili ya wajasiriamali wote wakubwa, wa
kati na wadogo ili kuwawezesha kiujuzi na kiushindani katika soko la
biashara” alisema Bi. Issa.
Aidha
Bi. Issa amesema kuwa siku hiyo kutakuwa na kliniki ya biashara kwa
watu wote kutoka kwa wataalamu wa biashara ili kuweza kuwapatia mafunzo
wajasiriamali wakubwa na wadogo ili waweze kupata mafanikio yao na jamii
kwa ujumla kupitia biashara zao.
Kwa upande wa Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Sekta Binafsi nchini (TPSF) Bw. Godfrey Simbeye amesema kuwa maonesho hayo yatawajengea wajasiriamali fursa za masoko kwa biashara nchini na Afrika kwa ujumla.
“Kupitia
maonesho hayo wajasiriamali watapata fursa ya kutengeneza masoko ya
biashara zao kwa ubora zaidi nchini na afrika kwa ujumla ili waweze
kujitangaza kimataifa” alisema Bw. Simbeye.
Aidha
Bw. Simbeye amesema kuwa wana mpango wa kuwaelimisha wajasiriamali kwa
wingi zaidi ili waweze kuwa wabunifu na kukuza uchumi wa nchi kupitia
sekta ya biashara ndani na nje ya Tanzania.
Mbali
na hayo Mkurugenzi Simbeye amesema kuwa anawakaribisha watu wote
wajasiriamali wakubwa na wadogo kufika katika maonesho hayo ambayo
hayana kiingilio ili waweze kupata ujuzi wa kutosha kwa maendeleo ya
biashara zao na kuinua uchumi wa nchi.
0 comments:
Post a Comment