Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Na. Lilian Lundo - MAELEZO - Dodoma
Serikali kupitia Mpango wa Kuinua Ubora wa Elimu Tanzania (EQUIP-T)
imefanikiwa kupunguza utoro katika Shule ya Msingi Uhelela iliyoko
Wilayani Bahi mkoani Dodoma kupitia mafunzo ya usimamizi wa shule
wanayopewa wajumbe wa Kamati za Shule za Msingi Mkoani humo.
Mwenyekiti wa Kamati ya Shule hiyo Isaya Chimela aliyasema hayo,
Wilayani Bahi wakati wa mahojiano na timu ya Mpango wa Kuinua Ubora wa
Elimu ya Wilaya hiyo .
"Utoro wa wanafunzi hapa shuleni kwetu umepungua baada ya sisi wajumbe
wa Kamati ya Shule kupatiwa mafunzo ya usimamizi wa shule kupitia
EQUIP-T . Pia, tumeweka zamu za wajumbe kufuatilia mahudhurio ya
wanafunzi shuleni mara mbili kwa wiki, " alifafanua Chimela.
Aidha aliendelea kwa kusema kuwa ufuatiliaji wa karibu wa mahudhurio kwa
wanafunzi wa shule hiyo ndiyo uliyopelekea kupungua kwa kiwango cha
utoro kwa wanafunzi hao.
Vile vile Kamati hiyo imekuwa ikiwaelimisha wazazi ambao watoto wao ni
watoro, juu ya umuhimu wa elimu kwa watoto wao na namna ambavyo watoto
hao watafanikiwa ikiwa watapata elimu.
Kutokana na elimu hiyo wazazi wamekuwa wakishirikiana na Kamati hiyo
katika kufuatilia mahudhurio na maendeleo ya taaluma ya watoto wao.
Kwa upande wake Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo Dankan Kamwela amesema kuwa
shule hiyo imefanikiwa kupunguza utoro kutoka wanafunzi 127 (30%) kwa
siku mwaka 2015 hadi wanafunzi 12 (8%) kwa siku mwaka 2016.
Home »
» Mafunzo ya Wajumbe wa Kamati ya Shule ya Msingi Uhelela Yapunguza Idadi ya Wanafunzi Watoro.
0 comments:
Post a Comment