Na Ismail Ngayonga
MAELEZO
Dar es Salaam
28.10.2016
WADAU
wa habari nchini wametakiwa kuzingatia maslahi ya taifa na tansia ya
habari kwa mapana zaidi kuhusu muswada wa sheria ya huduma za habari wa
mwaka 2016, kwa kuwa muswada huo umekusudia kuboresha maslahi yao.
Hayo yamesemmwa leo Jijini Dar es Salaam na Kaimu Katibu Mkuu wa Chama cha UDP, Goodluck
Ole Medeye katika mahojiano maalum na mwandishi wa habari hizi wakati
akitoa msimamo wake kuhusu maudhui ya muswada huo.
Medeye
alisema muswada huo umekuja katika wakati mwafaka ikiwemo muswada
umekusudia kuanzishwa kwa vyombo maalum vya kusimamia tasnia ya habari
ikiwemo vyombo vya maadili, maslahi, haki, na usalama wa waandishi wa
habari.
Kwa
mujibu wa Medeye alisema muswada huo hauna budi kuungwa mkono na wadau
kwa kuwa umelenga kuboresha maslahi ya wanahabari ikiwemo sharti la
kisheria la kuwataka wamiliki wa vyombo vya habari kuwakatia bima ya
afya na mifuko ya hifadhi ya jamii.
Aidha
Medeye alisema muswada huo ni vyema ukaongeza kipengele cha kuwataka
wamiliki kuajiri waandishi wa kudumu katika vyombo vya habari, kwani
wengi wa waandishi waliopo katika tasnia hiyo ni wawakilishi pekee,
ambao mmiliki hawajibiki nae.
“Uhuru
wa kweli katika tasnia ya habari utapatikana pale ambapo, maslahi yao
yataboreshwa ikiwemo suala zima la utoaji wa bima na maslahi mengine,
ambayo katika muswada huu yamewekwa wazi zaidi” alisema Medeye.
Aidha
Medeye alisema kupitishwa kwa muswada huo kutaiwezesha fani ya habari
kuendelea kuheshimika na kuaminika zaidi kama zilivyo fani za udaktari,
uuguzi, sheria na kadhalika.
MWISHO
0 comments:
Post a Comment