Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com
Home » » OLE MEDEYE: MUSWADA WA HABARI UMEKUSUDIA KUBORESHA MASLAHI YA WANAHABARI

OLE MEDEYE: MUSWADA WA HABARI UMEKUSUDIA KUBORESHA MASLAHI YA WANAHABARI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

Na Ismail Ngayonga
MAELEZO
Dar es Salaam
28.10.2016
WADAU wa habari nchini wametakiwa kuzingatia maslahi ya taifa na tansia ya habari kwa mapana zaidi kuhusu muswada wa sheria ya huduma za habari wa mwaka 2016, kwa kuwa muswada huo umekusudia kuboresha maslahi yao.

Hayo yamesemmwa leo Jijini Dar es Salaam na Kaimu Katibu Mkuu wa Chama cha UDP, Goodluck Ole Medeye katika mahojiano maalum na mwandishi wa habari hizi wakati akitoa msimamo wake kuhusu maudhui ya muswada huo.

Medeye alisema muswada huo umekuja katika wakati mwafaka ikiwemo muswada umekusudia kuanzishwa kwa vyombo maalum vya kusimamia tasnia ya habari ikiwemo vyombo vya maadili, maslahi, haki, na usalama wa waandishi wa habari.

Kwa mujibu wa Medeye alisema muswada huo hauna budi kuungwa mkono na wadau kwa kuwa umelenga kuboresha maslahi ya wanahabari ikiwemo sharti la kisheria la kuwataka wamiliki wa vyombo vya habari kuwakatia bima ya afya na mifuko ya hifadhi ya jamii.

Aidha Medeye alisema muswada huo ni vyema ukaongeza kipengele cha kuwataka wamiliki kuajiri waandishi wa kudumu katika vyombo vya habari, kwani wengi wa waandishi waliopo katika tasnia hiyo ni wawakilishi pekee, ambao mmiliki hawajibiki nae.

“Uhuru wa kweli katika tasnia ya habari utapatikana pale ambapo, maslahi yao yataboreshwa ikiwemo suala zima la utoaji wa bima na maslahi mengine, ambayo katika muswada huu yamewekwa wazi zaidi” alisema Medeye.

Aidha Medeye alisema kupitishwa kwa muswada huo kutaiwezesha fani ya habari kuendelea kuheshimika na kuaminika zaidi kama zilivyo fani za udaktari, uuguzi, sheria na kadhalika.

MWISHO

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa