Na Jovina Bujulu
MAELEZO
Dar es Salaam
WANATASNIA
ya habari nchini wametakiwa kuunga mkono uanzishwaji sheria ya huduma
za habari nchini kwa kuwa muswada uliopo umekusudia kutoa mafunzo
yanawasaidia kuwaongezea weledi katika utendaji wao wa kazi.
Hayo
yamesemwa na Mkurugenzi wa Habari, Hassan Abbas wakati wa ziara yake ya
kutembelea vyombo vya habari leo Jijini Dar es Salaam, ambapo alitoa
ufafanuzi kuhusu maudhui yaliyopo katika muswada wa sheria hiyo.
Aliongeza
kuwa mafunzo hayo yatatolewa ndani na nje ya nchi na hivyo kuwasaidia
waandishi wa habari wa Tanzania kubadilishana uwezo na ujuzi na wenzao
kutoka nchi mbalimbali duniani.
Mafunzo hayo yatakuhusisha mafunzo ya muda mrefu na mfupi, warsha, makongamano na semina.
Abbas
alisema kuwa mfuko huo utakuza programu za uendelezaji wa maudhui ya
ndani na nje ya nchi na kuchangia utafiti na maendeleo katika nyanja za
habari na mawasiliano ya umma.
Kwa
mujibu wa Abbas fedha za mfuko huo zitaidhinishwa na Bunge, misaada na
michango mbalimbali ya hiari kutoka vyombo vya habari.
Aidha
Abbas alisema waandishi wa habari kupitia mfuko huo watajengewa uwezo
kwenye nyanja mbalimbali ikiwemo kilimo, afya, uchumi, elimu na
kadhalika ili kuwawezesha kuripoti na kuandika habari hizo kwa weledi
zaidi.
0 comments:
Post a Comment