Na Ally Daud-Maelezo
0744953136
MIKOA na halmashauri nchini zimetakiwa kuweka tahadhari
juu ya ugonjwa wa kipindupindu kwa kuzingatia usafi binafsi na usafi wa mazingira
hasa wakati wa mvua za vuli na msimu wa sikukuu za mwisho wa mwaka ili kuweza kuepuka
ugonjwa huo.
Hayo yamesemwa
na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Ummy Mwalimu wakati
wa mkutano na waandishi wa habari kuhusu mwenendo wa ugonjwa wa kipindupindu kwa
mwezi Novemba 2016 uliofanyika jijini Dar es salaam.
“Mikoa na Halmashauri zote nchini ziwe katika hali
ya tahadhari juu ya ugonjwa wa kipindupindu kwa kuzingatia usafi binafsi na usafi
wa mazingira hasa wakati wa mvua za vuli na msimu wa sikukuu za mwisho wa mwaka
ili kuweza kuepuka ugonjwa huo” alisema Waziri Ummy.
Aidha Waziri Ummy amesema kuwa Mikakati ya kudhibiti
ugonjwa wa Kipindupindu ishirikishe sekta mbalimbali za afya nchini bila kusahau
jamii husika na kuhakikisha kila Halmashauri inaunda na kuimarisha Kamati ya
Afya ya Kata.
Aidha Waziri Ummy ameiagiza
Mikoa na Halmashauri zote nchini kutoa taarifa ya wagonjwa wapya wa Kipindupindu
ili jitihada za makusudi za kupambana na ugonjwa huo zifanyike mapema ili kujenga
taifa lisilo na magonjwa ya mlipuko.
Mbali na hayo Waziri Ummy amesema kuwa takwimu zinaonesha
katika mwezi Novemba 2016 jumla ya mikoa sita ikiwemo Morogoro yenye wagonjwa
282, Dodoma 96 na vifo 2, Mara 31, Kigoma 30 na vifo 4, Arusha 11 na Dar Es
Salaam 8 kutoka wagonjwa 250 na vifo 4
kwa mwezi Oktoba mwaka huu.
Kwa wakati huohuo Waziri Ummy amepokea vifaa vya matibabu
ya mabadiliko ya awali ya Saratani ya mlango wa kizazi vyenye thamani takribani
milioni 100 za kitanzania kutoka Shirika la Kimataifa la Pink Ribbon Red Ribbon
ili kupambana na ugonjwa huo nchini.
Akikabidhi msaada huo Mtendaji Mkuu wa Shirikahilo
Bi. Celina Schocken amesema kuwa wametoa vifaa hivyo ili kuisaidia nchi kwa juhudi
za kimakusudi katika kupambana na ugonjwa wa saratani ili kuokoa maisha ya
wanawake wa Tanzania.
“Tumeamua kutoa vifaa hivi ili kuisaidia nchi kwa juhudi
za kimakusudi katika kupambana na ugonjwa wa saratani ili kuokoa maisha ya
wanawake wa Tanzania ”alisema Bi. Schocken.
MWISHO
0 comments:
Post a Comment