Home » » SERIKALI KUPITIA UPYA KODI ZINAZOLETA KERO

SERIKALI KUPITIA UPYA KODI ZINAZOLETA KERO

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Benny Mwaipaja, WFM, Dar es salaam
WAZIRI wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango, amesema kuwa Serikali imeanza kuyafanyia kazi maoni na malalamiko ya wafanyabiashara na wawekezaji kwa ujumla kuhusu kodi zinazolalamikwa kwa lengo la kuhuisha ama kubadili kodi zinazoonekana kuwa ni kero
Dkt Mpango amesema hayo mara baada ya kutembelea na kukagua maonesho ya kwanza ya viwanda vya ndani, yanayofanyika katika Uwanja wa maonesho ya biashara wa Mwalimu J. K. Nyerere, barabara ya Kilwa, Jijini Dar es salaam.
Amewataka wafanyabiashara na wawekezaji kuwasilisha maoni yao kuanzia mwezi huu wa Desemba wakati ambapo Serikali kupitia Wizara ya Fedha na Mipango, iko katika mchakato wa kuandaa Bajeti ya Mwaka wa Fedha 2017/2018.

0 comments:

 
Supported byBlogs za Mikoa
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa