Home » » DOKTA MPANGO AWATAKA WATANZANIA KUWASADIA WATU WENYE ULEMAVU

DOKTA MPANGO AWATAKA WATANZANIA KUWASADIA WATU WENYE ULEMAVU

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Benny Mwaipaja, WFM, Dar es salaam
WAZIRI wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango, ameitaka jamii kuwasaidia watu wenye ulemavu ili waweze kujiajiri na kukabiliana na hali ngumu ya maisha.
Dkt. Mpango ametoa rai hiyo wakati alipotembelea banda la mlemavu asiyeona, Bw. Abdalah Nyangalilo, ambaye amewakusanya watu kadhaa wenye ulemavu na kuwapatia mafunzo ya ushonaji nguo katika maonesho ya kwanza ya viwanda vya ndani, yanayofanyika katika Uwanja wa maonesho ya biashara wa Mwalimu J. K. Nyerere, barabara ya Kilwa, Jijini Dar es salaam.
Waziri huyo wa Fedha na Mipango, ambaye ametoa msaada wa vyerehani viwili ili kuwaongezea nguvu, amesema kuwa watu wenye ulemavu wanaweza kufanya mambo makubwa ya kijasiliamali yatakayo wasaidia kujikimu kimaisha, endapo jamii itajitolea kuwasaidia kwa hali na mali

0 comments:

 
Supported byBlogs za Mikoa
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa