Na. Lilian Lundo - MAELEZO
Watanzania wameaswa kutodharau bidhaa zinazotengenezwa ndani ya nchi na kukimbilia bidhaa za nje ya nchi.
Waziri
wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango ameyasema hayo leo, alipotembea
banda la Shirika la Maendeleo ya Viwanda Vidogovidogo (SIDO) katika
maonyesho ya viwanda vya Tanzaniaa yanayoendele Uwanja vya Mwalimu J. K. Nyerere (Saba Saba), Jijini Dar es Salaam.
Dkt.
Mpango amesema kuwa Tanzania haitaweza kuwa nchi ya viwanda ikiwa
watanzania wenyewe hawathamini bidhaa zinazotengenezwa ndani ya nchi.
“Ili tufanikiwe katika uchumi wa viwanda lazima tuanze kwa kile tunachoweza kwa kutumia rasilimali tulizonazo ndani ya nchi,” alifanunua Dkt. Mpango.
Aliendelea
kwa kusema kuwa, watanzania wengi wanadharau mashine ambazo
zinatengenezwa na SIDO ambazo gharama yake ni nafuu ukilinganisha na
mashine zinazotengenezwa nje ya nchi.
Vile
vile amesema kuwa haiwezekani hata jembe la mkono liagizwe toka nje ya
nchi wakati kuna viwanda ndani ya nchi ambavyo vinauwezo wa kutengeneza
majembe yenye ubora.
Aidha ameishauri SIDO kutengeneza mashine nyingi na kusambaza nchi nzima ili watanzani waweze kujiajiri na hata kufungua viwanda vidogo vidogo kwa kutumia mashine hizo.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya
Maendeleo ya Biashara Tanzania (TANTRADE) Edwin Rutageruka amesema
kwamba maonyesho hayo yanafanyika kwa mara ya kwanza na yatakuwa ni
endelevu ambapo yatakuwa yakifanyika kila mwaka mwezi Desemba
yakiambatana na maadhimisho ya Uhuru wa Tanzania Bara.
Ameeleza
kuwa, lengo la monyesho hayo ni kubadilishana uzoefu na kutoa fursa
katika sekta ya viwanda, kutoa hamasa kwa watanzania kununua bidhaa za
ndani ya nchi, kuunganisha wazalishaji na wenye malighafi, kuwawezesha
watafiti na wabunifu kuonana na wenye viwanda, kutoa fursa kwa
watanzania kujua palipo na viwanda pamoja na kuwawezesha vijana na
wanafunzi kujiajiri wenyewe kwa kuanzisha viwanda.
0 comments:
Post a Comment