Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com
Home » » BULEMBO,PROFESA KABUDI WATEULIWA KUWA WABUNGE

BULEMBO,PROFESA KABUDI WATEULIWA KUWA WABUNGE

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
RAIS John Magufuli ameteua wabunge wawili wapya wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akiw2mo msomi maarufu nchini, Profesa Palamagamba Kabudi na Mwenyekiti wa Taifa wa Jumuiya ya Wazazi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Abdallah Bulembo.
Kwa mujibu wa taarifa ya Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu jana kwa vyombo vya habari, pia Rais Magufuli amemteua Benedicto Martin Mashiba kuwa Balozi.
“Wabunge wateule hawa wataapishwa kwa taratibu za Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,” ilieleza taarifa ya Ikulu na kuongeza kuwa kituo cha kazi na tarehe ya kuapishwa kwa Balozi mteule Mashiba itatangazwa baadaye.
Uteuzi wa wabunge hao wawili, Profesa Kabudi na Bulembo unafanya Rais Magufuli afikishe idadi ya wabunge wanane kati ya 10 ambao kikatiba anaruhusiwa kuwateua.
Wengine ambao aliwateua kuwa wabunge na kisha kuwateua kuwa mawaziri ni Profesa Makame Mnyaa Mbarawa (Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano), Balozi Dk Augustine Mahiga (Mambo ya Nje ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki), Dk Philip Mpango (Fedha na Mipango), Profesa Joyce Ndalichako (Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi), Dk Abdallah Possi (Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, Watu Wenye Ulemavu).
Mwingine ni Dk Tulia Ackson ambaye ni Naibu Spika wa Bunge. Kwa upande wa wasifu wa Profesa Kabudi, ni Mhadhiri Mwandamizi katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam akiwa katika Bodi ya Uongozi inayotawala kuanzia mwaka 2015 hadi 2018 akiwa na wadhifa wa Mwanasheria na Katibu wa Bodi hiyo ya Uongozi.
Alikuwa Mjumbe wa Bunge la Katiba lililokaa na kupitisha Rasimu ya Katiba Inayopendekezwa mwaka 2015, na amekuwa mmoja wa wasomi wanaotegemewa katika nyanja mbalimbali nchini, lakini akiwa gwiji katika masuala ya sheria.
Aidha, wasifu wa Profesa Kabudi unaonesha kuwa Julai 5, mwaka jana, aliteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya Maendeleo ya TIB, lakini akiwa pia na nyadhifa mbalimbali katika vyama vya kitaaluma na taasisi za kidini.
Kwa upande wa Bulembo, mbali ya kuwa Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi ya CCM Taifa ambayo inamfanya moja kwa moja kuwa Mjumbe wa Kamati Kuu na Halmashauri Kuu ya Taifa ya chama hicho tawala, alikuwa miongoni mwa wajumbe 32 wa Kamati ya Kumnadi mgombea wao wa urais mwaka 2015, Dk John Magufuli, lakini akapewa jukumu la kuwa Mratibu akitembea na mgombea huyo kwa muda wote wa kampeni iliyozaa ushindi wake Oktoba 25, 2015.
Kabla ya kuwa Mwenyekiti wa Wazazi Taifa, Bulembo alikuwa Mjumbe wa Baraza Kuu la Utekelezaji la jumuiya hiyo, na ameshikilia nyadhifa mbalimbali za uongozi kutoka katika ngazi za chini ikiwamo kuwa Diwani wa Kata ya Nyasho katika Manispaa ya Musoma mkoani Mara.
Aidha, Bulembo anafahamika kuwa mwanamichezo maarufu nchini, akiwahi kuwa Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya kilichokuwa Chama cha Soka Tanzania (FAT) katika miaka ya mwishoni mwa 1990, na pia kiongozi wa Chama cha Soka Mkoa wa Mara (FAM). Mtoto wa Bulembo, Halima Bulembo pia ni Mbunge
 CHANZO GAZETI LA HABARI LEO

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa