NA Daudi Manongi - MAELEZO.
17/01/2017
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Hassan Suluhu
anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika maadhimisho ya mwaka mpya wa kichina
yatakayofanyika katika viwanja vya Mnazi Mmoja tarehe 21 na 22 January
2017 kuanzia saa tatu asubuhi mpaka saa 11 Jioni.
Hayo
yamesemwa leo jijini Dar es Salaam na Mkuu wa Kituo cha Utamaduni wa
China nchini Bw.Gao Wei alipokuwa akizungumza na waandishi wa Habari.
Amesema
mwaka huu utafahamika kama mwaka wa Jogoo wenye kuweka mtazamo mkubwa
Afrika huku yakiambatana na burudani nyingi kutoka kwa vikundi
mbalimbali vya sanaa kutoka China na nchini,maonyesho ya picha,vyakula
vya kichina na maonyesho mbalimbali ya kibiashara.
Katika
maadhimisho hayo makampuni 60 yatashiriki katika kuonyesha bidhaa
mbalimbali,pia nchi 150 na majiji 400 yatasherehekea maadhimisho haya ya
mwaka mpya.
Akizungumzia
mahudhurio ya siku hiyo Bw.Wei amesema kuwa wanategemea ushiriki wa
watu zaidi ya 6000 katika maadhimisho hayo ya siku mbili ambayo
yanasisitiza zaidi urafiki na mshikamano.
Katika kufanikisha maadhimisho hayo Kampuni za HUAWEI na CRDB Benki zimejitokeza kudhamini maadhimisho ya mwaka huu.
0 comments:
Post a Comment