Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com
Home » » SERIKALI YAUNDA TUME KUCHUNGUZA KUUNGUA KWA CHUMBA CHA MIZIGO UWANJA WA NDEGE JIJINI DAR ES SALAAM

SERIKALI YAUNDA TUME KUCHUNGUZA KUUNGUA KWA CHUMBA CHA MIZIGO UWANJA WA NDEGE JIJINI DAR ES SALAAM

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
 Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa (katikati), akiwa na viongozi mbalimbali wakiwemo wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) wakati akitoka kukagua chumba namba cha kuhifadhia mizigo kilichoungua moto jana usiku.

 Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa (katikati), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari kuhusu hatua zilizofikiwa na serikali baada ya kutokea moto huo. Kulia ni Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Gabriel Migile na kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Profesa Ninatubu Lema.
 Mkutano na wanahabari ukiendelea. 

 Paa la chumba kilichoungua.
 Waandishi wa habari wakiangalia chumba hicho.
 Chumba namba mbili cha kutunzia mizigo Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), kikiwa kimetekea kwa moto uliotokea jana usiku katika uwanja huo.
wanahabari wakichukua taarifa hiyo.

Na Dotto Mwaibale

SERIKALI imeunda tume ya watu 12 kwa ajili ya kuchunguza tukio la kuungua moto chumba namba mbili cha kuhifadhia mizigo katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA).

Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa alisema tume hiyo itaongozwa na Mwenyekiti wa Bodi wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Joseph Nyahende.

"Tume hiyo tumeipa muda wa mwezi mmoja ili kukamilisha uchunguzi huo ambapo tutatoa taarifa kamili ya chanzo cha moto huo" alisema Mbarawa.

Akizungumzia kuhusu tukio hilo alisema moto huo ulitokea jana usiku kwenye chumba namba mbili cha kuhifadhia mizigo ya abiria katika uwanja huo hata hivyo thamani ya vitu vilivyoungua bado haijajulikana.

Katika hatua nyingine Waziri Mbarawa ameinyoonyea kidole kampuni inayofanya kazi ya kupokea mizigo katika uwanja huo ya Swissport kuwa iache kufanya njama za kuzuia kampuni ya Nas Dar Airco iliyopewa mkataba wa kazi katika uwanja kufanya kazi vinginevyo serikali itaifutia leseni.

"Tunataarifa kuwa nyinyi Swissport mnaizuia kampuni hiyo kufanya kazi nasema badilikeni vinginevyo tutawafutia leseni yenu" aliagiza Profesa Mbarawa.

Profesa Mbarawa alitoa maagizo kwa kampuni hiyo ianze kufanya kazi haraka iwezekanavyo kama walivyokubaliana katika mkataba waliopewa.

Mkurugenzi Mkuu wa Swissport Mrisho Yassin hakuweza kuzungumzia suala hilo kwa wakati huo kutokana na mazingira yaliyokuwepo baada ya mkutano huo na alipopigiwa simu baadaye muda wote simu yake ilikuwa ipo bize.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa