Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com
Home » » MAKONDA AKABIDHI MAJINA MENGINE 97 KWA KAMISHNA MKUU WA MAMLAKA YA KUZUIA NA KUPAMBANA NA DAWA ZA KULEVYA SIANGA

MAKONDA AKABIDHI MAJINA MENGINE 97 KWA KAMISHNA MKUU WA MAMLAKA YA KUZUIA NA KUPAMBANA NA DAWA ZA KULEVYA SIANGA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 



Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda,  akionyesha majina mengine 97 ya wafanyabiashara wa Dawa za Kulevya awamu ya tatu wakati akimkabidhi majina hayo Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya, Rogers William Sianga, kwa ajili ya kuyafanyia kazi. Makonda alikabidhi majina hayo leo mchana wakati wa mkutano na waandishi wa habari uliofanyika kwenye Ukumbi wa Mwalimu Nyerere (JNCC) jijini Dar es Salaam, ambapo alisema kuwa majina ya awamu hii ya tatu yatatikisa nchi kwani wameanzia toka uongozi wa awamu ya tatu iliyoongozwa na Rais Mstaafu,Benjamini Mkapa, ya nne Rais Mstaafu Jakaya Mrisho Kikwete na hii ya Tano inayoongozwa na Rais Dk. John Pombe Magufuli.
CHANZO MAFOTO BLOG



Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda akikabidhi majina mengine 97 ya awamu ya tatu kwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya, 
Rogers William Sianga 
ili yaanze kushughulikiwa.

Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda akizungumza katika mkutano huo amekabidhi majina mengine 97 ya awamu ya tatu kwa Bw. Rogers William sianga kuwa kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya ili yaanze kushughulikiwa.


Shekh wa Mkoa wa Dar es salaam na Mwenyekiti wa Kamati ya Amani Alhadi Mussa akizungumza na watendaji mbalimbali wa vyombo vya ulinzi na usalama mkoa wa Dar es salaam pamoja na viongozi mbalimbali wa Chama cha Mapinduzi, Wenyeviti wa serikali za mitaa na madiwani pamoja na vijana mbalimbali waliokuwa wanatumia dawa za kulevya katika mkutano wa taarifa ya maendeleo ya Kampeni ya kupiga vita dhidi ya madawa ya kulevya.


Msanii wa muziki wa kizazi kipya, Khalid Mohamed, TID, akizungumza na kutoa ushuhuda, na kuahidi kutoa ushirikiano katika Vita ya kupambana na madawa ya kulevya.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA


Mchungaji Geoge Fupe akizungumza katika mkutano huo wa KKKT Dayosisi ya Mashariki na Pwani.

Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Mh. Paul Makonda akizungumza jambo na Bw. Rogers William sianga kuwa kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya katika mkutano wa kutoa tathmini ya kampeni ya kutokomeza madawa ya kulevya Kamishna katika mkoa wa Dar es salaam.

Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda akiwa pamoja na viongozi wengine wakiwa katika mkutano huo.

Kamanda wa Kanda Maalum ya Dar es salaam Kamishna Saimon Sirro akizungumzo wakati akitoa taarifa ya kampeni hiyo leo.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa