Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb) (kulia) akieleza kuhusu juhudi za Serikali katika kutengeneza mazingira mazuri ya kibiashara wakati wa mkutano na Mjumbe wa Waziri Mkuu wa Uingereza anayeshughulikia Biashara Bw. Lord Hollick katika ukumbi wa Wizara hiyo jijini Dar es salaam.
Wajumbe wa Mkutano walioongozana na Mjumbe wa Waziri Mkuu wa Uingereza anayeshughulikia Biashara Bw. Lord Hollick, wakisikiliza kwa makini maelezo ya Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb) (hayupo pichani), kuhusu umuhimu wa kufanya biashara ya bidhaa zilizoongezwa thamani ili kukuza viwanda vya ndani, wakati wa mkutano huo jijini Dr es salaam.
Mjumbe wa Waziri Mkuu wa Uingereza anayeshughulikia Biashara Bw. Lord Hollick (kushoto) akifafanua jambo wakati wa Mkutano kati yake na Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb) (hayupo pichani) kuhusu nia ya kuwekeza katika ujenzi wa Uwanja wa ndege wa Msalato Dodoma, Kulia ni Balozi wa Uingereza nchini Tanzania Bi. Sarah Cooke, Mkutano uliofanyika Makao Makuu ya Wizara jijini Dar es salaam.
Mjumbe wa Waziri Mkuu wa Uingereza anayeshughulikia Biashara Bw. Lord Hollick (kulia) akisisitiza kuhusu kuendelea kuimalisha uhusiano wa kibiashara kati ya Tanzania na Uingereza huku Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb) (kushoto) akimsikiliza kwa makini katika ukumbi wa Wizara hiyo jijini Dar es salaam.
Waziri
wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango ameitaka nchi ya Uingereza
kutazama uwezekano wa kufanya biashara na Tanzania kwa kununua bidhaa
zilizoongezwa thamani badala ya hali ya sasa ambapo nchi hiyo imekuwa
ikinunua bidhaa ghafi ilihali ikiingiza nchini bidhaa zake za viwandani.
Dkt.
Mpango ameyasema hayo alipokutana na Mjumbe wa Waziri Mkuu wa Uingereza
anayeshughulikia masuala ya Biashara Bw. Lord Hollick ailipo tembelea
Makao Makuu ya Wizara hiyo jijini Dar es salaam.
Amesema
Tanzania inataka kuona inauza bidhaa zake zenye thamani ambazo
zitatokana na maendeleo makubwa ya viwanda hapa nchini ikiwa ni Sera ya
nchi kuwa na uchumi wa kati unaotegemea viwanda ifikapo mwaka 2025.
Nchi
ya Uingereza imekuwa ikifanya biashara na Tanzania kwa kiasi kikubwa na
takwimu zinaonesha nchi hiyo inaingiza bidhaa zenye thamani mara nane
ya Tanzania jambo ambalo linatakiwa kurekebishwa ili biashara iwe na
manufaa kwa pande zote mbili.
Miongoni
mwa bidhaa ghafi ambazo zimekuwa zikisafirishwa kwenda uingereza ni
pamoja na Chai, kahawa na madini ya vito huku Uingereza ikiingiza bidhaa
za viwandani zenye thamani kubwa ikijumuisha mashine (mitambo),vifaa
vya umeme, bidhaa za plastiki na madawa.
0 comments:
Post a Comment