TAARIFA KWA
UMMA
Waziri wa
Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye ameteua Kamati Maalum
ya Hamasa kuelekea Mashindano ya AFCON chini ya umri wa miaka 17
yatakayofanyika mwezi May 2017 nchini Gabon ambapo Tanzania inawakilishwa na
Timu ya Taifa ya Mpira wa Miguu ya Vijana (Serengeti Boys).
Kamati
hiyo yenye jumla ya wajumbe nane itaongozwa na Mwenyekiti Charles Hillary
kutoka Azam Tv na Katibu wake Selestine Mwesigwa ambaye pia ni katibu Mkuu wa
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) na wajumbe wa kamati hiyo ni Dkt
Hassan Abass Mkurugenzi Idara ya Habari MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali,
Ruge Mutahaba Mkurugenzi wa Vipindi na Uzalishaji kutoka Clouds Media Group,
Hoyce Temu Mrembo wa Tanzania mwaka 1999, Maulid Kitenge Mtangazaji kutoka EFM,
Beatrice Singano Mkurugenzi wa Mawasiliano Airtel Tanzania, Erick Shigongo
Mkurugenzi wa Global Publishers na wasanii wa muziki wa kizazi kipya Ali Kiba na
Naseeb Abdul (Diamond Platinumz).
Imetolewa na
Zawadi Msalla
Kaimu
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini,
Wizara
ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo.
28/02/2017
0 comments:
Post a Comment