Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com
Home » » ‘DAWA ZA UZAZI HAZINA MADHARA’

‘DAWA ZA UZAZI HAZINA MADHARA’

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

Imeandikwa na Lucy Lyatuu 
HAKUNA madhara yoyote katika matumizi ya dawa za uzazi wa mpango hivyo, jamii iache dhana potofu inayosababisha kuwepo kwa matumizi madogo ya dawa hizo nchini; imesema Serikali.
Mratibu wa Usalama wa Dawa za Uzazi wa Mpango Kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk Cosmas Swai aliyasema hayo jana jijini Dar es Salaam wakati akizungumzia kuhusu matumizi ya dawa hizo na umuhimu wake katika kupanga idadi ya watoto watakaozaliwa.
Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Idadi ya Watu Duniani (UNFPA) linaadhimisha siku hiyo kesho katika Viwanja vya Mwembeyanga ambapo Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk Hamis Kigwangala atakuwa mgeni rasmi.
Alisema matumizi sahihi ya dawa hizo yanaweza kuzuia hata magonjwa mbalimbali ya uzazi ikiwemo saratani ya shingo ya uzazi na kwamba kila anayetumia dawa hizo na kuona kuna dalili ambazo hazifurahii afike katika kituo chochote cha afya ili kupewa ushauri zaidi. Alisema katika kipindi cha mwaka jana Serikali imetumia juma ya dola za Kimarekani milioni 19 kununua dawa za uzazi wa mpango.
CHANZO HABARI LEO

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa