Mwaka jana Serikali ilitangaza dhamira ya kupiga marufuku ya kuzalisha,
kuuza, kusambaza, uingizaji na matumizi ya mifuko ya plastiki ya
kubebea bidhaa nchini kutokana na uchafuzi wa mazingira. Kwa kuwa hatua
hiyo ni kubwa, Serikali imeamua kuwashirikisha wadau na wananchi ili
kupata maoni yao. Kwahiyo, wananchi wote wanaotaka kutoa maoni kuhusiana
na hatua hiyo wanakaribishwa katika mkutano wa wazi wa kupokea maoni
utakaofanyika siku ya Jumamosi tarehe 22 mwezi Julai 2017 kuanzia saa
tatu asubuhi katika ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam. Mkutano
huo umeandaliwa na Ofisi ya Makamu wa Rais na utahudhuriwa na Waziri wa
Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira),Mhe. January
Makamba (MB). Karibuni wote mtoe maoni na sauti yenu isikike.
Home »
» KIKAO CHA WAZI CHA KUTOA MAONI DHAMIRA YA SERIKALI KUPIGA MARUFUKU MATUMIZI YA MIFUKO YA PLASTIKI NCHINI
KIKAO CHA WAZI CHA KUTOA MAONI DHAMIRA YA SERIKALI KUPIGA MARUFUKU MATUMIZI YA MIFUKO YA PLASTIKI NCHINI
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
0 comments:
Post a Comment