Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com
Home » » KIKAO CHA WAZI CHA KUTOA MAONI DHAMIRA YA SERIKALI KUPIGA MARUFUKU MATUMIZI YA MIFUKO YA PLASTIKI NCHINI

KIKAO CHA WAZI CHA KUTOA MAONI DHAMIRA YA SERIKALI KUPIGA MARUFUKU MATUMIZI YA MIFUKO YA PLASTIKI NCHINI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 


 
Mwaka jana Serikali ilitangaza dhamira ya kupiga marufuku ya kuzalisha, kuuza, kusambaza, uingizaji na matumizi ya mifuko ya plastiki ya kubebea bidhaa nchini kutokana na uchafuzi wa mazingira. Kwa kuwa hatua hiyo ni kubwa, Serikali imeamua kuwashirikisha wadau na wananchi ili kupata maoni yao. Kwahiyo, wananchi wote wanaotaka kutoa maoni kuhusiana na hatua hiyo wanakaribishwa katika mkutano wa wazi wa kupokea maoni utakaofanyika siku ya Jumamosi tarehe 22 mwezi Julai 2017 kuanzia saa tatu asubuhi katika ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam. Mkutano huo umeandaliwa na Ofisi ya Makamu wa Rais na utahudhuriwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira),Mhe. January Makamba (MB). Karibuni wote mtoe maoni na sauti yenu isikike.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa