Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Katibu Mtendaji wa BASATA,Godfrey Mngereza akiwa na Mkurugenzi wa TOT,Gasper Tumaini.
Wasanii wa Kikundi cha Kaole wakimkaribisha Katibu Mtendaji wa BASATA,Godfrey Mngereza katika tamasha la SHIWATA.
Msanii maarufu nchini,Bakari Mbelemba (Mzee Jangala) na wageni wengine akifuatilia kwa karibu maonesho ya wasanii.
Washiriki wa tamasha wakifuatilia kwa karibu maonesho ya wasanii.
Wasanii wa Kaole wakicheza ngoma mbele ya wageni waalikwa.
Mbunge Zungu akituza kikundi cha ngoma za asili cha Sangura.
MBUNGE
wa Ilala,Mussa Azzan Zungu ameahidi kutoa mifuko 100 ya saruji kwa
ajili ya kujengea nyumba za wasanii wa Mtandao wa Wasanii Tanzania
(SHIWATA).
Akizungumza
wakati wa kufunga tamasha la siku mbili lililowakutanisha wasanii zaidi
ya 600 kutoka vikundi mbalimbali vikiwemo vya Tanzania One Theatre
(TOT)Zungu alisema ametoa saruji hiyo ili kuwasaidia SHIWATA kuendeleza
juhudi za kuwakomboa wasanii kwa kuwajengea makazi.
Mbunge
Zungu pamoja ya kushuhudia michezo mbalimbali alishindwa kujizuia
kuungana na wasanii kucheza na kutunza ngoma ya asili ya Sangura kutoka
kabila la Wapogoro mkoani Morogoro.
>Bendi
za muziki wa dansi za Hisia Sound ya Abdul Salvador,bendi ya TOT na
Umoja Sound ziliwakonga wasanii na wengine waliohudhuria tamasha hilo.
Katika
tamasha hilo lililofunguliwa na Katibu Mtendaji wa Baraza la Sanaa
Tanzania (BASATA) Godfrey Mngereza wasanii wa fani mbalimbali walionesha
vipaji vyao vya kucheza sarakasi,ngoma za asili,maigizo,muziki wa
dansi,muziki wa asili na taarabu.
Mbunge
wa Mkuranga, Abdallah Ulega ambae tamasha hilo awali lilikuwa lifanyike
kijiji cha Wasanii Mkuranga na baadaye kuhamishiwa jijini Dar es
Salaam kutokana na mvua ya msimu uliopita kuharibu barabara ya kwenda
kijijini alisema jutihada zifanyike ili mwakani lifanyike Mkuranga.
> > > > >
Mkurugenzi
wa TOT,Gasper Tumaini alisema tamasha hilo limefana na wao wako tayari
kushirikiana na SHIWATA katika matamasha mengine.
Pamoja
ya kudhaminiwa na Kampuni ya SBC inayotengeneza soda za Pepsi, Kampuni
ya Simu ya TTCL kulikuwa na msaada wa kisheria wa kujikinga na magonjwa
ya UKIMWI.
0 comments:
Post a Comment