Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com
Home » » MBUNGE WA TEMEKE ALALA RUMANDE

MBUNGE WA TEMEKE ALALA RUMANDE

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

Na. Raymond Kaminyoge, Mwananchi
 
Mbunge wa Temeke, Abdallah Mtolea yuko rumande tangu jana baada ya kukamatwa na Polisi akituhumiwa kuendesha gari ambalo bima yake ilikuwa imeisha muda.
Akithibitisha kukamatwa kwake leo Alhamis Julai 20, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Temeke, Gilles Mrosso amesema mbunge huyo yuko rumande tangu jana jioni.
Amesema amekamatwa na askari wa usalama barabarani Temeke akiendesha gari ambalo bima yake ilikuwa imeisha muda wake.
“Askari wa usalama barabarani walipomhoji aliamua kuwapuuza na kuondoka zake,” amesema.
Amesema polisi walimfuatilia na kumkamata na sasa anaendelea kuhojiwa ili aweze kufikishwa mahakamani.
“Atafikishwa mahakamani kama tunavyofanya kwa raia yoyote, nafasi yake kama mbunge haiwezi kuwa sababu ya kutofuata sheria,” amesema.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa