KAWAIDA:-
NAIBU Katibu Mkuu wa CCM Bara, Rodrick Mpogolo
ameipongeza Benki ya NMB kwa kuanzisha akaunti ya Fanikiwa kwani ina
lengo la kuwagusa watu wa kipato cha chini ambao ndiyo sehemu kubwa ya
wananchi wa Tanzania. Mpogolo ameyasema hayo baada ya kutembelea banda
la benki ya NMB kwenye maonesho ya Saba Saba ambapo alipata fursa ya
kupata elimu kuhusu bidhaa na huduma mbalimbali zinatolewa na benki hiyo
kubwa nchini.
Aidha, alisema kuwa akaunti hiyo ni nzuri kwa sababu ni mahususi kwa
ajili ya wafanya biashara wadogo wadogo wakiwemo mama lishe, wakaanga
chips, wauza magenge n.k ambao ni sehemu kubwa ya Watanzania. Akaunti
hii pia inamwezesha mfanyabishara kutambulika kama mteja mfanya
biashara, atakua mwanachama kweye klabu za biashara za NMB (NMB Business
Club), itamwezesha kupata mkopo mpaka milioni thelathini, ina gharama
nafuu za uendeshaji na ni rahisi kuifungua kwani haihitaji nyaraka
nyingi. Lakini pia mteja anaweza kupata huduma katika matawi zaidi ya
200 ya NMB yaliyoenea nchi nzima.
“Akaunti ya Fanikiwa inalenga kuwasaidia wafanyabiashara wadogo ili
waweze kukuza mitaji na kuendeleza kipato chao; mtu anapopata nafasi ya
kupata mkopo ni njia ya kuongeza kipato cha familia na ndivyo uchumi wa
taifa unavyoweza kujengwa, Mimi niwapongeze benki ya NMB kwa kuanzisha
akaunti hii na niwahamasishe Watanzania watumie fursa hii kuweza
kuongeza kipato kwa ajili ya maisha yao na waweze kukuza uchumi wa nchi
yetu,” alisema Mpogolo.
Vilevile, Mpogolo aliwaasa wananchi wasiogope kuchukua mikopo kwenye
mabenki ili waweze kuongeza kipato, “Ni jukumu la kila mtu kumuhamasisha
mwenzake aone benki ni mahali anapoweza kupata fursa za kujikomboa
kiuchumi, kuendeleza ustawi wake kwani mambo kama haya zamani hayakuwepo
ambayo yanagusa watu wa hali ya chini.”
“Binafsi jambo lililonigusa ni kuanzishwa kwa akaunti ambayo inagusa
watu wa kipato cha chini, naona kwamba Benki ya NMB inakwenda kuwa
mkombozi wa watu wanyonge kwa kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Rais
na serikali yake ya kuona wananchi wa kawaida na wao wanaboresha uchumi
wao.”
0 comments:
Post a Comment