Imeandikwa na Mohammed Mussa
ASKARI wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Marwa
Wambura (25) amepandishwa katika kizimba cha Mahakama ya hakimu mkazi
Kinondoni kwa tuhuma za kuua.
Akisomewa mashitaka hayo kwa mara ya kwanza katika Mahakama hiyo,
mbele ya hakimu Isic Kuppa, mwendesha mashitaka Joseph Nasua alidai kuwa
Juni 17, 2017, maeneo ya Kibamba CCM, wilaya ya Ubungo jijini Dar es
Salaam, mtuhumiwa Rashid Sadick alitenda kosa hilo huku akijua kufanya
hivyo ni kinyume cha sheria.
Mshitakiwa hakutakiwa kujibu chochote kutokana na mahakama hiyo kutokuwa na uwezo wa kusikiliza shitaka hilo.
CHANZO HABARI LEO
0 comments:
Post a Comment