KAMANDA wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Ilala, Salum Hamduni ameieleza
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa mshitakiwa Hassan Nuru,
anayekabiliwa na mashitaka ya wizi wa mafuta ya petroli na dizeli yenye
thamani ya Sh milioni 239, kuwa aliwatoroka akiwa Kituo Kikuu cha Polisi
Dar es Salaam.
Hamduni alitoa madai hayo jana mbele ya Hakimu Mkazi, Huruma Shaidi
baada ya Wakili wa Serikali, Salum Msemo kudai kuwa kesi hiyo imekuja
kwa ajili ya kusikilizwa. Alidai mshitakiwa huyo ambaye pia
alijitambulisha kama Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Hashi Energy (T)
Ltd alitakiwa kurejesha kielelezo ambacho ni malori matatu ya mafuta ili
polisi waendelee na upelelezi.
Alidai, Januari 2015 akiwa Mkuu wa Upelelezi Mkoa wa Kipolisi Ilala,
alipokea mafaili yenye makosa ya jinai likiwemo la wizi wa mali
isafirishwayo kutoka kwa Kamishna Msaidizi wa Polisi, ACP David
Mnyambugha. Akiongozwa na Wakili Msemo, Kamanda huyo alidai yalitoka
maagizo kwamba kielelezo kilichopokelewa na Nuru kirudishwe Polisi
ambayo ni malori matatu yenye mafuta ya petroli na dizeli na kwamba
Februari 14, 2015 aliandika barua kwa Kampuni ya Hashi ili kurudisha
vielelezo hivyo walivyopewa na Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai.
Pia alidai, katika barua hiyo aliielekeza kampuni hiyo irudishe
kielelezo hicho ifikapo Februari 16, 2015 ikiwa ni pamoja na kumpigia
simu Nuru kwa kuwa yeye ndiye aliyekabidhiwa kielelezo hicho. Aliendelea
kudai kuwa kilelezo hakijarudishwa na badala yake mshitakiwa alifika
ofisini kwake na wakili wake ambapo aliwaelimisha kuwa kielelezo
walipewa kwa ajili ya kutunza na kinapohitajika kinatakiwa kurudishwa.
Alieleza wakati wanatoka ofisi ya Mkuu wa Upelelezi, kabla ya kuingia
katika ofisi yake, walimuona mshitakiwa akiongea na simu na kwamba yeye
na wakili wake wakaendelea na kuingia ofisi na walipotazama nyuma
hawakumuona mshitakiwa huyo
CHANZO HABARI LEO.
0 comments:
Post a Comment