Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Tunapenda kutoa taarifa kwa Ndugu, Jamaa, Marafiki, Familia na wote tuliopatwa na msiba huu wa marehemu Professor Henslay William Kabisama uliyotokea huko Ontario, California, Marekani.
Mwili wa mpendwa wetu Prof Henslay Kabisama utawasili Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam leo Ijumaa Julai 21, 2017 saa tisa mchana. Tunaombeleza nyumbani kwa marehemu Ursino Victoria nyuma ya Ofisi za Halotel.
Mazishi yatafanyika kesho Jumamosi Julai 22, 2017 yakitanguliwa na Ibada ambayo itafanyika katika kanisa la St Alban Upanga saa saba kamili mchana. Baada ya hapo tutaelekea makaburi ya Kinondoni kwa mazishi.
Bwana alitoa na bwana ametwaa
Jina la Bwana libarikiwe
AMEN.
0 comments:
Post a Comment