Benny Mwaipaja, WFM-Dar es Salaam
Zikiwa
zimebaki siku tatu kati ya siku 15 zilizoongezwa na Serikali kwa
wananchi kulipa kodi ya majengo bila adhabu, baadhi ya wakazi wa Jiji la
Dar es Salaam wameiomba Serikali iongeze muda mwingine zaidi ili watu
wote waweze kulipa kodi hiyo bila adhabu kutokana na changamoto
mbalimbali zilizojitokeza wakati wa zoezi hilo.
Wananchi
hao wamemweleza Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango
alipofanya ziara za kushitukiza katika Ofisi za Mamlaka ya Mapato
Tanzania TRA-Mtaa wa Kipata-eneo la Mnazi Mmoja na Mbagala mkoani Dar es
Salaam
Wamesema
kuwa mwamko wa wananchi kulipa kodi ni mkubwa hali iliyosababisha
foleni kubwa kila mahali nchini kutokana na uhaba wa watumishi wa TRA
pamoja na vitendeakazi muhimu kama vile kompyuta na mashine za
kielektroniki za kutolea risiti (EFDs).
0 comments:
Post a Comment