Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com
Home » » Kampuni ya Kuja na Kushoka Tools yaiunga mkono Serikali ya awamu ya tano

Kampuni ya Kuja na Kushoka Tools yaiunga mkono Serikali ya awamu ya tano

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Na: Paschal Dotto - MAELEZO
Kampuni ya “Kuja Na Kushoka Tools Manufactures Group” imeunga mkono jitihada za serikali utunzaji mazingiza na kuwa na uchumi wa kati kupitia viwanda kwa kubuni mashine inayotengeneza nishati ya mkaa mbadala kwa kutumia mabaki ya mazao na takataka badala ya kukata miti.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dare es salaam, Mkurugenzi wa kampuni hiyo Bw. Leonard Kushoka amesema kuwa ugunduzi huo utarahisisha matumizi ya nishati hiyo ambayo ni mkombozi kwa wananchi wa kipato cha kati na chini.  

“Teknolojia hii ni njia mbadala na salama kwa mazingira kwani inatumia taka za aina zote pamoja na mabaki ya mazao badala ya kukata miti, vilevile ni njia ya utunzaji wa mazingira kutokana na takataka hizo kutumika  katika kuzalisha mkaa kwa matumizi ya nyumbani”. Alisema Kushoka.

Bw. Kushoka ameongeza kuwa katika miji mikubwa  kama Dar es salam, Mwanza na Arusha matumizi ya nishati ya mkaa ni makubwa kutokana na kuwa na idadi kubwa ya watu ikiwa  jiji la Dar es salam pekee matumizi ya mkaa yanafikia magunia 28,000 kwa siku sawa na asilimia 50 ya mkaa wote unaozalishwa nchini ikifuatiwa na Mwanza na Arusha.

Aidha Bw.Kushoka alisema kuwa mashine hiyo yenye uwezo wa kuzalisha magunia 20 ya mkaa kwa siku inatumia nishati ya mafuta ya dizeli au umeme kutegemea na matakwa ya mteja na inauzwa kwa shilingi milioni 15.

Bw. Kushoka aliongeza kuwa licha ya mashine hiyo kulinda mazingira pia inaongeza thamani ya mazao kwani mabaki yote ya mazao yanatumiwa na mashine hiyo kuzalishia mkaa mbadala kama malighafi.

Kampuni hii ilianzishwa mwaka 2000 mkoani Tabora kwa lengo la kutunza mazingira kwa kutumia teknolojia ya kisasa na inafanya kazi kw karibu na Wakala wa Huduma za Misitu (TFS) pamoja na Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa