Na: Paschal Dotto - MAELEZO.
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh.Samia Suluhu Hassan,
amesema kuwa serikali inaendelea kuhakikisha Mahakama hazijihusishi na
vitendo vya rushwa ili kutoa haki kwa mujibu wa Sheria.
Mh.
Samia ameyasema hayo Jijini Dar es Salaam alipokuwa akifungua mkutano
wa Chama cha majaji na mahakimu wa nchi za Jumuiya ya Madola uliofanyika
katika ukumbi wa Benki Kuu ya Tanzania.
‘Ninaamini,
nia ya kujenga mahakama bora na yenye kuaminika kwa Tanzania haiwezi
kutenganishwa na juhudi za serikali katika kuondoa umaskini na rushwa”
amesisitiza Mh.Samia.
Aidha
Makamu wa rais amesema kuwa kuna uhitaji mkubwa kwa nchi kuwa na
mahakama huru, makini na yenye kuwajibika ipasavyo kwani mahakama huru
ni msingi mzuri wa demokrasia.
Alisema
kuwa pamoja na changamoto mbalimbali za mahakama uhuru wa mahakama
ambao ni umakini,uwajibikaji na utoaji haki kwa kufuata utawala wa
sheria kwa wananchi wake uko palepale.
Kwa
upande wa Tanzania Mhe. Samia amesema kuwa katika awamu ya tatu ya
mapambano dhidi ya rushwa ambapo kwa awamu mbili zilizopita serikali
imefanikiwa kwa kiasi kikubwa kupunguza malalamiko yaliyotokana na
ukiukwaji wa haki.
Katika
awamu ya tatu ya mkakati wa kupambana na rushwa utakaochukua miaka
mitano kuanzia 2017 hadi 2022, Tanzania itachukua uzoefu kutoka kwenye
mkuatno huu wa kimataifa kutoka kwa nchi wanachama wa Jumuiya ya madola.
Kwa
upande wake Jaji mkuu wa Tanzania Professa Ibrahim Juma alisema
mahakama hiyo iko huru na inatekeleza majukumu yake pasipo kuingiliwa
na mtu yeyote na akaahidi kuendelea kubadilishana uzoefu na mahakama za
nchi wanachama ili kuboresha utendaji kazi.
Aidha
Profesa Juma amesema Mahakama ya Tanzania kupitia majaji imekubaliana
kuwa kila Jaji atatakiwa kuhukumu zaidi ya kesi 220 ambazo ni asilimia
38 ya kesi zilizoahirishwa mwaka 2012 hadi asilimia 5 Desemba 2016 na
hii itafanyika kila mwaka ili kujipima wao wenyewe kama moja ya malengo
waliyojiwekea.
Akizungumzia
mipango ya mahakama hiyo Profesa Juma amesema kuwa hadi kufikia mwaka
2020 mahakama hiyo itakuwa imekamilisha ujenzi wa mahakama Kuu
13,mahakama za hakimu mkazi 14,mahakama za Wilaya 48,pamoja na mahakama
za Mwanzo 100.
Mkutano
wa mwaka huu wa chama cha majaji na mahakimu wa nchi za jumuiya ya
madola umefanyika kwa mara ya kwanza hapa nchini tangu Tanzania ijiunge
na chama hicho mwaka 1970.
0 comments:
Post a Comment