Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com
Home » » MAKONDA ATAKA MABAHARIA KUFICHUA MAGENDO

MAKONDA ATAKA MABAHARIA KUFICHUA MAGENDO

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 Imeandikwa na Lucy Ngowi
MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amewataka mabaharia na manahodha wa meli nchini kushirikiana na serikali kufichua wanaoingiza mizigo ya magendo na dawa za kulevya kupita ukanda wa bahari.
Makonda alisema hayo jana alipokuwa akifungua warsha ya mafunzo ya Sheria ya Kazi ya Mwaka 2006 kwa mabaharia jijini Dar es Salaam. Alisema endapo eneo la bahari litakuwa na wazawa, watatoa taarifa kwa serikali kuhusu uhalifu unaoendelea huko, hali itakayosaidia kufahamu shughuli haramu za uvuvi zinazoendelea katika bahari.
“Mabaharia wanaweza kutoa taarifa muhimu kuhusu dawa zinazopitishwa baharini kwani serikali imekuwa ikishughulika na suala hilo ili kulidhibiti. Tusaidieni tujiepushe na hatari kubwa inayokabili kizazi chetu. Pia kwenye mali za magendo ambazo hazilipiwi kodi,” alisema Makonda.
“Ubaharia ni kazi muhimu katika kuchochea ukuaji wa uchumi wa taifa kupitia Ukanda wa Bahari, mabaharia wanapaswa kuona wana jukumu la kuchangia ukuaji wa pato la taifa,” alisema Makonda.
Akisoma risala kwa niaba ya wenzake, Aloyce Mpazi alisema wanakosa ajira katika meli na kampuni zinazofanya utafiti na uchimbaji wa mafuta na gesi Mtwara, Tanga na maeneo mengine tofauti na nchi nyingine zinazotoa kipaumbele cha ajira kwa mabaharia wao.
CHANZO HABARI LEO 

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa