Home » » NDIKUMANA KATAUTI AFARIKI DUNIA GHAFLA

NDIKUMANA KATAUTI AFARIKI DUNIA GHAFLA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
 Imeandikwa na Mwandishi Wetu
Aliyekuwa Kocha Msaidizi wa Timu ya Soka ya Rayon Sports nchini Rwanda, Hamad Ndikumana Katauti amefariki dunia ghafla leo hii. Kwa mujibu wa Afisa Habari wa Rayon Sports Gakwaya Olivier, amesema muda mfupi uliopita kwamba kifo cha Ndikumana kilisababishwa na ugonjwa wa moyo.
“Alisikia maumivu makali kifuani akaomba soda ya baridi wakamletea na alipomaliza kunywa tu kidogo akatapika na akaishiwa pumzi na ndipo akakata kauli,” alisema Olivier na kuongeza kwamba bado wanasubiri uchunguzi wa madaktari.
Ndikumana ambaye amewahi kucheza soka Tanzania akiwa na klabu ya Stand United, amewahi kuwa mume wa muigizaji Irene Uwoya na wana mtoto mmoja.
CHANZO HABARI LEO 

0 comments:

 
Supported byBlogs za Mikoa
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa