Home » » UFANYE NINI UKIGUNDUA UMENUNUA ARDHI ILIYOWEKWA REHANI BILA KUJUA ?.

UFANYE NINI UKIGUNDUA UMENUNUA ARDHI ILIYOWEKWA REHANI BILA KUJUA ?.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

Na Bashir Yakub.

Umenunua kiwanja au nyumba. Aliyekuuzia amekuhahakikishia kuwa kiwanja/nyumba hiyo iko salama na haina mgogoro wowote. Mbali na mgogoro pia amekuhakikishia kuwa kiwanja/nyumba hiyo hajaiweka rehani popote ili kuchukua mkopo. 

Amekuhakikishia kuwa mpaka wakati unanunua kiwanja/nyumba hiyo, ni kuwa iko salama na haijashikiliwa na benki au taasisi yoyote ya fedha kwa ajili ya mkopo.

Au pengine hukuuliza kabisa kama kuna deni lolote, umejikuta tu umenunua bila kuuliza swali kama hilo. Baadae sasa ndio unagundua kuwa kiwanja/nyumba uliyonunua kuna taasisi moja ya fedha ambapo aliyekuuuzia alichukua mkopo na kuiweka dhamana/rehani na bado hajamalizia mkopo huo. 

Taasisi hiyo inakuonesha nyaraka halali za kushikilia kiwanja/nyumba hiyo kama dhamana muda mrefu hata kabla wewe hujanunua. Na kwa bahati mbaya aliyekuuzia hujui tena alipo au bahati nzuri unajua alipo.

Lakini hata ukijua alipo, tayari umeishanunua na hela ulishampa na kila kitu kilikwishakamilika. Nini kinakusaidia kukutoa katika hali hii ambayo sasa unaelekea kuingia katika mgogoro mkubwa wenye sura ya hasara. 

Sheria namba 4 ya 199, Sheria ya ardhi itatupatia majibu ya jambo hili.

1.UNUNUZI WA AINA HIYO UNAVYOTAMBULIKA KISHERIA.

Ununuzi wa aina hiyo unatambulika kama aina ya ununuzi ambao unaingilia haki ya mtoa mkopo. Kifungu cha 69(1) cha sheria hiyo kinauita ununuzi huo kama ununuzi unaolenga kupora/kuharibu(defeat) haki ya mtoa mkopo. 
Mtoa mkopo hapa ni benki au taasisi nyingine ya fedha iliyotoa mkopo. 
Kwahiyo kujikuta umenunua eneo lenye mazingira ya namna hiyo hadhi yake ni kama ilivyoelezwa hapa juu.

0 comments:

 
Supported byBlogs za Mikoa
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa