Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com
Home » » DR MASHINJI (KATIBU MKUU) AZUNGUMZIA NAFASI YA UENYEKIITI NDANI YA CHADEMA

DR MASHINJI (KATIBU MKUU) AZUNGUMZIA NAFASI YA UENYEKIITI NDANI YA CHADEMA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Katibu Mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dkt. Vicent Mashinji amefunguka kuhusu nafasi ya uenyekiti ndani ya chama hicho.

Mwanasiasa huyo amesema mwanachana yeyote wa Chadema anaweza kuwa Mwenyekiti ila kwa sasa ni wakati wa Freeman Mbowe ambaye ndiye anashikilia nafasi hiyo.

“Chadema ni chama ambacho kina fursa na kila mtu na mwanachama yeyote anaweza kuwa Mwenyekiti lakini watu waelewe huu si wakati wake ni zamu ya Mhe. Freeman Mbowe ukifika wakati wa uchaguzi atakuja mtu mwingine,” amesema Dkt. Mashinji.

“Mfumo wetu ni tofauti na CCM, chama kinaongozwa na Mwenyekiti ambaye ni Rais amevaa kofia mbili kwa utawala bora hili haliwezekani sababu chama kinatakiwa kuongozwa na Mwenyekiti ambaye anatakiwa pia kuisimamia Serikali,” ameongeza.

Pia amesema toka miaka ya 90 Mhe. Mbowe alikuwa Mwenyekiti wa vijana lakini watu wanasahau kuwa bado hiki ni kipindi cha uongozi wake na bado haujamalizika.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa