Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com
Home » » PROF. KAMUZORA- WAFANYAKAZI WA OFISI YA MPIGA CHAPA WA SERIKALI WATAKIWA KUCHAPA KAZI NA KUWA WABUNIFU

PROF. KAMUZORA- WAFANYAKAZI WA OFISI YA MPIGA CHAPA WA SERIKALI WATAKIWA KUCHAPA KAZI NA KUWA WABUNIFU

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera na Uratibu) Prof. Faustin Kamuzora akifurahia kazi nzuri inayofanywa na Mpiga Chapa Mkuu wa Serikali alipofanya ziara fupi kiwandani hapo jijini Dar es Salaam tarehe 20 Februari 2018.
 Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera na Uratibu) Prof. Faustin Kamuzora akisikiliza kwa makini maelezo kutoka kwa Kaimu Mpiga Chapa Mkuu wa Serika alipotembelea kiwanda hicho na kukutana na wafanyakazi jijini Dar es Salaam tarehe 20 Februari 2018.
  Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera na Uratibu) Prof. Faustin Kamuzora akiongea na wafanyakazi wa kiwanda cha Mpiga Chapa Mkuu wa Serikali, (katikati) Kaimu Mpiga Chapa Mkuu wa Serikali Bw. John Kaswalala, jijini Dar es Salaam tarehe 20 Februari 2018. 

Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera na Uratibu) Prof. Faustin Kamuzora awataka watumishi wa ofisi ya Mpiga Chapa Mkuu wa Serikali  kujituma na wawe wabunifu ili kuzalisha kwa ufanisi zaidi.
Amesema hayo alipotembelea kiwanda cha Mpiga Chapa Mkuu wa Serikali kilichopo jijini Dar es salaam,tarehe 20 Februari 2018.
Amewasisitiza wafanyekazi kwa nguvu, wajue vifaa wanavyotumia na kuvielewa ili kuweza kufanya kazi kwa urahisi na kuepuka uharibifu wa mashine hizo, watambue kuwa Serikali inazidi kuboresha mazingira ya kazi na taratibu za kuendesha shuguli zake za kiuchumi.
“Tunaishi katika ulimwengu wa maarifa,hivyo maarifa tuyatumie kazini kwa kuwa wabunifu na kufahamu vizuri mitambo na vifaa tunavyotumia ili tuweze kuzalisha kwa ufanisi ili wote tufaidike na matunda ya uzalishaji huo.” Alisema Prof. Kamuzora.
Akielezea juu ya uendeshaji shughuli za kiwanda hicho Kaimu Mpiga Chapa Mkuu wa Serikali Bw. John Kaswalala alisema, kiwanda hicho kinaendelea kukua kiuchumi na kuimarika. Aidha, watumishi wa Mpiga Chapa Mkuu wa Serikali wamempongeza sana Prof. Kamuzora kwa utendaji wake na kufika kwake katika ofisi zao, na kuomba serikali izidi kuwawezesha kwa vifaa, mitambo na teknolojia ili wazidi kuzalisha zaidi.
Imetolewa na Ofisi ya Waziri Mkuu
Dar es Salaam, 21 Februari, 2018

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa