Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com
Home » » WASOMI, WANAHARAKATI WAPINGA MABADILIKO NSSF, PPF

WASOMI, WANAHARAKATI WAPINGA MABADILIKO NSSF, PPF



Gabriel Mushi na Elizabeth Mjatta, Dar es Salaam

WAKATI Kituo cha Haki za Binadamu (LHRC), kikipanga kuiburuza Serikali mahakamani kupinga matumizi ya Sheria za Mifuko ya Hifadhi ya Jamii,wasomi nao wamepinga sheria hiyo kwa kudai ni kandamizi.


Hatua hiyo, imekuja baada ya Bunge kuifanyia marekebisho na hatimaye Rais Jakaya Kikwete kuisani Aprili 13, 2012 kwa ajili ya kuanza kutumika rasmi.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini Dar es Salaam jana, wakati uzinduzi wa ripoti ya haki za binadamu ya nusu mwaka, Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo hicho, Hellen Kijo Bisimba, alisema sheria hiyo ni kandamizi kwa wafanyakazi wote kwa sababu haikushirikisha hata wafanyakazi wenyewe ambao ni ndiyo wadau wakuu.

Alisema kipengele cha fao la kujitoa kifutwa na badala yake mwanachama apokea mafao yake, baada kufikisha umri wa kustaafu kwa hiari (miaka 55) au kwa lazima (miaka 60).

“Kwa sababu katika mazingira halisi ya nchi yetu, muda wa kuishi kwa mtu ni miaka 45, sasa kama asipofikisha miaka 55 ina maana mafao yake yatapotea… huu ni ufisadi uliofanywa kwa maslahi yao binafsi kwa sababu kama tunavyojua, fedha hizi zinatumika kwenye miradi yao kama ile ya NSSF, ilivyojenga Chuo Kikuu cha Dodoma na sasa mradi wa Kigamboni.

“SSerikali inatakiwa kuzipitia upya sheria kama hizi, kwa sababu hata tulipoangalia kwenye rekodi za Bunge, sheria hii ilipitishwa kinyemel… kwa msingi huo tumejipanga kwenda mahakamani kupinga matumizi ya sheria hii,” alisema.

Kwa upande wake Mhadhiri Mwandamizi wa Idara ya Siasa kutoka Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam, (UDSM), Dk. Benson Bana, ameiponda sheria hiyo na kusema si rafiki wa wafanyakazi.

Aliiitaka Serikali kuacha kuingilia mifuko ya Hifadhi ya Jamii, kwani inaonekana inailazimisha mifuko hiyo kutekeleza majukumu yake.

“Mifuko hii inatakiwa iwe huru, kwa sababu wana hisa ni wafanyakazi wenyewe…kama ni kujenga miradi iache mifuko hii ijipangie yenyewe na si Serikali jamani,” anasema Dk.Bana.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Chama Cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (TAMWA), Ananilea Nkya alisema sheria hiyo inatakiwa kufutwa mara moja..

“Kwa maoni yangu, hii sheria inatakiwa ifutwe mara moja ina mkandamiza mfanyakazi…kwasababu wapo watu ambao baada ya kuwa katika ajira kwa muda fulani, wanataka kujiajiri sasa unasemaje mtu kama huyo asipewe mafao yake,”alisema Nkya.

Mbunge wa Kilwa Kaskazini, (CCM) Murtaza Mangungu, aliunga mkono hatua ya Rais Kikwete na Bunge kupitisha marekebisho ya sheria hiyo na hivyo kuwataka Watanzania kukubaliana na mabadiliko hayo.

“Tunatakiwa kujifunza, tuwe na tabia ya kujiwekea akiba, kwa sababu sheria hii inawataka wananchi wawe na tabia ya kujiwekea akiba ndio maana hata sisi wabunge tumeipitisha.

“Hapa wanashindwa kuelewa, kwa mfano nchi kama Marekani wananchi wake wanaruhusiwa kuchukua mafao yao wakishafikisha miaka 62 vile vile

Chanzo: Mtanzania



0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa