na Happiness Mnale
JUMUIYA
ya Kikristo Nchini (CCT), imevijia juu viwanda vya kuzalisha dawa za kupunguza
makali ya virusi vya ukimwi (ARV’s) duniani, na kusema vina siri ya tiba ya
ugonjwa huo, lakini vimeamua kukaa kimya.
Akizungumza
jana jijini Dar es Salaam wakati wa ufunguzi wa semina ya siku mbili ya waandaaji
wa vipindi vya redio na runinga vitakavyohusiana na masuala ya kuondoa
unyanyapaa, Makamu Mwenyekiti wa CCT, Askofu Valentino Mokiwa, alisema siri
hiyo ni ya kushindwa kuzalisha dawa za kutibu kabisa ugonjwa huo, ili waweze
kuendelea kufanya biashara kupitia ARV’s.
Alisema
ugonjwa huo umetumika kuwanufaisha watu wenye viwanda kwa kuufanya ni mradi.
Aidha,
aliwataka watafiti wa Kikristo kuongeza kasi ya kuleta tiba na kuondoa hofu ya
ugonjwa huo.
Akizungumzia
suala la unyanyapaa; Mokiwa alisema kanisa litahakikisha linaondoa hali hiyo
kwani lina wajibu kwa jamii.
Pamoja
na hayo, aliitaka serikali kutunga sheria za kumlinda mwathirika kutokana na
unyanyapaa, hasa maeneo ya maofisi.
Naye
Rogers Steven, ambaye anaishi na virusi vya ukimwi alisema ameishi na ugonjwa
huo kwa miaka 15 sasa.
Alisema
amekutana na hali ya juu ya unyanyapaa ndani na nje ya familia, na kuwataka
Watanzania kuwafariji wagonjwa kwa kuwaonyesha upendo.
Mwanamke aibiwa mtoto
na Efracia Massawe
MKAZI
wa Buguruni kwa Mnyamani, jijini Dar es Salaam, Hadija Omari (37), ameibiwa
mtoto wake mwenye umri wa miaka miwili na nusu na mwanamke asiyefahamika.
Akizungumza
na Tanzania Daima jijini Dar es Salaam jana, Hadija, alisema mwanae huyo
aitwaye Sabrina Hamisi, aliibwa Novemba 11, mwaka huu.
Hadija,
alisema siku hiyo akiwa katika biashara yake ya mama lishe eneo hilo, alifika
mteja mwanamke na kuagiza chakula na kumwandalia, kisha kutoka nje.
Alisema
aliporudi ndani katika hali ya kushangaza hakumkuta mteja huyo wala mtoto wake.
Mama
huyo alisema kuwa, ametoa taarifa Kituo cha Polisi Buguruni na kupewa jalada
lenye namba BG/MNY/RB/ 1922/12.
Anamuomba
msamaria yeyote atakayefanikiwa kumuona mtoto huyo kuwasiliana naye kwa simu
namba 0718203086 na 0654988856 au afike katika ofisi za gazeti hili zilizopo
Mtaa wa Mkwepu maeneo ya Posta, Dar es Salaam.
CHANZO MTANZANIA DAIMA
0 comments:
Post a Comment