Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com
Home » » Serikali sasa kupata unafuu wa mikopo

Serikali sasa kupata unafuu wa mikopo

Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe, amesema Serikali itapunguza gharama za kukopa fedha kwa riba katika taasisi za fedha na benki nchini, baada ya Benki ya Rasilimali (TIB) kuingia makubaliano na Benki ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika, katika kutoa mikopo isiyokuwa na riba kwa miradi yote ya maendeleo ikiwamo ya sekta ya uchukuzi.
Dk Mwakyembe aliyasema hayo jana wakati benki hizo mbili ziliposaini mkataba wa ushirikiano mwema wa kuwekeza katika sekta ya uchukuzi.
Alisema kupitia ushirikiano huo, Serikali itapunguza kukopa katika benki na taasisi za fedha zenye riba kubwa na badala yake, itatumia fursa hiyo kukopa kutoka TIB kwa ajili ya miradi yote ya maendeleo ikiwemo miundombinu.
Alisema hiyo itasaidia kupunguza mzigo mkubwa kwa Serikali katika kukopa.
“Kusaini kwa makubaliano haya ni mapinduzi makubwa hapa nchini kwa sababu Serikali itapata unafuu katika bajeti yake,” alisema.
Dk Mwakyembe alisema katika kipindi cha mwaka 2005 hadi sasa Benki ya DBSA, imetoa Dola 130 milioni za Marekani katika miradi ya miundombinu, huduma za kifedha, huduma za usafirishaji na mawasiliano hapa nchini.
Mkurugenzi Mkuu wa TIB, Peter Noni, alisema kwa kipindi kirefu uongozi wa benki hiyo umekuwa katika majadiliano na DBSA kwa lengo la kupata fedha za kuendeshea miundombinu katika sekta ya uchukuzi.
Ofisa Mtendaji Mkuu wa DBSA, Patrick Dlamini alisema benki hiyo ni taasisi ya kifedha ya Serikali ya Afrika Kusini na kwamba imelenga katika kusaidia miradi mikubwa.
Chanzo;Mwananhi
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa