Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Wakurugenzi wawili wa Bohari Kuu ya Dawa (MSD), Meneja Ubora wa
Bodi Binafsi ya Maabara ya Afya na Msajili Msaidizi wake wamefikishwa
katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakikabiliwa na mashtaka saba ya
matumizi mabaya ya madaraka, uhujumu uchumi na kuisababishia Serikali
hasara ya Sh3.450 bilioni kwa kuingiza nchini vitendanishi feki
vinavyotumika katika upimaji wa VVU.
Mwendesha Mashtaka wa Taasisi ya Kuzuia na
Kupambana na Rushwa (Takukuru), Leonard Swai aliwataja washtakiwa
wanaokabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi Namba 8/2014 ni Mkurugenzi wa
Operesheni wa Kanda ya Kaskazini wa Bohari Kuu ya Dawa (MSD), Sylvester
Matandiko ambaye hakufika mahakamani,ambapo mshtakiwa mwingine ni Kaimu
Mkurugenzi Mkuu wa Bohari Kuu ya Dawa ( MSD), Sadiki Materu ambaye pia
anakabiliwa na kesi nyingine ya uhujumu uchumi Namba 5 / 2014.
Katika kesi hiyo Namba 5/2014, Materu, Ofisa
Mtendaji Mkuu wa Kiwanda cha Tanzania Pharmaceutical Industries Ltd
(TPI) kinachotengeneza Dawa za Kurefusha Maisha (ARV) nchini, Ramadhani
Madabida na wenzao watatu wanakabiliwa na mashtaka matatu likiwamo la
kusambaza dawa bandia za ARV na kusababisha hasara ya Sh148.3 milioni.
Wengine ni Meneja Ubora wa Bodi Binafsi ya Maabara
ya Afya, Zaynab Mfaume na Msajili Msaidizi wake, Joseph Nchimbi ambao
wote kwa pamoja wanakabiliwa na mashtaka ya kula njama, matumizi mabaya
ya madaraka, uhujumu uchumi na kuisababishia Serikali hasara ya Sh3.450
bilioni.
Wakili Swai alidai katika shtaka la kwanza, kuwa
kati ya Januari 20 na Julai 20, 2012 washtakiwa Matandiko, Materu,
Mfaume na Nchimbi wakiwa waajiriwa wa MSD na bodi binafsi ya maabara ya
afya walikula njama kwa kutumia madaraka yao vibaya kinyume na sheria.
Hata hivyo, washtakiwa walikana mashtaka dhidi
yao, Hakimu Hellen Liwa aliwataka washtakiwa hao kulipa nusu ya Sh3.450
bilioni ili waweze kuachiwa huru kwa dhamana, washtakiwa hao walishindwa
kukamilisha masharti hayo na kupelekwa rumande hadi Machi 6, 2014
watakaposomewa maelezo ya awali (PH).
Chanzo;Mwananchi
Chanzo;Mwananchi
0 comments:
Post a Comment