Home » » Wanachama CCM tusiwe waoga’ Wanachama CCM tusiwe waoga’

Wanachama CCM tusiwe waoga’ Wanachama CCM tusiwe waoga’

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mkoa wa Dar es Salaam, Abdilah Mihewa, amewataka wanachama wa chama hicho, Kata ya Msasani, kuacha woga wa kuwakabili wapinzani katika kipindi cha Uchaguzi wa Serikali za Mitaa baadaye mwaka huu.
Mihewa aliyasema hayo Dar es Salaam jana wakati akizungumza na Wenyeviti, Wajumbe wa Mashina wa kata hiyo.
Alisema viongozi wengi wa CCM ngazi ya chini ni waoga hasa wanapoulizwa na wapinzani chama chao kimeleta maendeleo gani kwa wananchi lakini wanashindwa kujibu wakati kazi iliyofanywa na CCM inaonekana kwa macho.
"Waelezeni wananchi mambo makubwa yaliyofanywa na chama tawala kupitia ilani yake ya mwaka 2010, CCM imejenga barabara za mitaa, imesogeza huduma za maji kwa wananchi hata kujenga shule za msingi na sekondari hivyo msikae kimya.
 "Upinzani hawana la kujivunia, kipindi hiki cha mchakato wa kupata Katiba Mpya, tuwe ngangari kwa kutoa maoni ya Serikali mbili ili kulinda Muungano wetu uliodumu miaka mingi," alisema.
Mihewa ambaye alikuwa mgeni rasmi katika mkutano ulioandaliwa na Diwani wa Viti Maalumu, Wilaya ya Kinondoni, Tatu Malyaga, pia alikabidhi vifaa vya michezo na vitendeakazi katika mashina ambavyo ni pamoja na bendera, kadi, jezi za mipira vikiwa na thamani ya sh. milioni 5.2.
Aliwataka wana CCM wa Msasani kuwa na umoja katika kipindi chote cha kuelekea Uchaguzi wa Serikali za Mitaa na Uchaguzi Mkuu ambapo makundi yaliyokuwepo mwaka 2009, 2010 yavunjwe ili wapate ushindi katika kata zote.
"Anayetaka kuendeleza makundi ndani ya chama aondoke kabisa kabla kipindi cha uchaguzi kukijafika, si jambo jema kwa kada wa CCM anayetaka uongozi atoe zawadi kwa wanachama na kama itabainika amefanya hivyo, ataadhibiwa," alisema.
Alimpongeza Malyaga kwa kuonesha moyo wa dhati wa kuwasaidia vijana na kutoa vitendea kazi kwani ni watu wachache wenye moyo wa kujitolea kama alivyofanya diwani huyo.

Chanzo;Majira

0 comments:

 
Supported byBlogs za Mikoa
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa