Home » » ‘Uchaguzi Serikali za Mitaa ufanyike mwakani’

‘Uchaguzi Serikali za Mitaa ufanyike mwakani’

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Taasisi isiyo ya Kiserikali ya Jukwaa la Katiba Tanzania imetoa mapendekezo kwa Serikali kuahirisha uchaguzi wa Serikali za mitaa ili ufanyike pamoja na uchaguzi mkuu mwakani.
Mwenyekiti wa taasisi hiyo, Deus Kibamba alisema uchaguzi huo unaotarajiwa kufanyika mwishoni mwa mwaka huu ni lazima uahirishwe kutokana na kucheleweshwa kwa ratiba ya mchakato wa Katiba Mpya.
Kibamba alisema, Katiba haiwezi kupatikana ndani ya muda uliokuwa umeahidiwa hapo awali na Rais Jakaya Kikwete Aprili 26, mwaka huu, kutokana na kubadilika kwa ratiba nzima ya mchakato huo.
Alisema kusogezwa mbele kwa uchaguzi huo kutatoa muda wa kuandaa sheria za kusimamia chaguzi hizo kwa kuwa Katiba Mpya pekee haitoshi kusimamia uchaguzi.
Aliongeza kuwa Jukwaa limependekeza nafasi za wagombea wa Serikali za mitaa kujumlishwa na zile za Uchaguzi Mkuu za Rais, mbunge na diwani. Zoezi hilo alisema litapunguza gharama za uchaguzi na muda ambao utatumika.
“Nchi jirani kama Kenya walikuwa nafasi sita za kupiga kura wakati wa uchaguzi mkuu mwaka jana na Zimbabwe walikuwa nafasi tano hivyo kwa Tanzania hilo linawezekana kabisa.”
Naye Mkurugenzi wa Sauti za Wanawake Walemavu Tanzania, Stella Jailos alisema ana wasiwasi kuwa Katiba Mpya haitakuwa na sura ya wananchi kutokana na wanasiasa kuutawala mchakato mzima wa kuipata.
Chanzo;Mwananchi 

0 comments:

 
Supported byBlogs za Mikoa
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa