Home » » Wahandisi nchini watahadharishwa

Wahandisi nchini watahadharishwa

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Wahandisi nchini wamekumbushwa kuwa makini kwa kutambua viashiria vya hatari na hasara zinazoweza kutokea katika miradi mbalimbali ya ujenzi wanayoisimamia.
Hayo yalisemwa na Mwezeshaji katika warsha ya wahandisi hao, Lwitiko Mwalukasa iliyokutanisha wahandisi kutoka vitengo mbalimbali nchini, zikiwamo idara za Serikali.
Aliwataka kuwa makini na viashiria hivyo, kwani baadhi vimesababisha hasara ya majanga, ambayo mengine huleta vifo na uharibifu wa mali.
Alisema kwa asili kazi ya uhandisi ni kubuni na kutengeneza kitu ambacho hakikuwapo awali, hivyo hutakiwa pia kufikiria kwamba hatari au hasara zinazoweza kutokana na vitu hivyo na jinsi ya kupambana nazo.
“Katika warsha hii tumewakumbusha hatua zote muhimu wanazopaswa kuzifuata kuanzia kipindi cha mradi unapopangwa kutekelezwa, kuangalia njia za kudhibiti viashiria vya hatari mapema, wengi wameonyesha kukubaliana na suala hili, hivyo tunaamini watawaelimisha na wengine katika maeneo yao ya kazi,”alisema Mwalukasa.
Alisema wahandisi hao iwapo watakuwa makini watasaidia mambo mengi ikiwa ni pamoja na kuwezesha miradi wanayoisimamia kukamilika kwa kiwango kinachokubalika na katika thamani ya fedha iliyotumika, hivyo kutimiza malengo ya kuanzishwa kwake.
Kwa upande wake, Rais wa Taasisi ya Wahandisi nchini, Dk Malima Mkandara alisema wameandaa warsha hiyo kuendelea kuwajengea uwezo wahandisi wa ndani ili waweze pia kushindana hadi kwenye soko la Kimataifa, hali kadhalika waweze kujipatia kazi za miradi mbalimbali ambayo inatekelezwa nje ya nchi.
 Chanzo;Mwananchi

0 comments:

 
Supported byBlogs za Mikoa
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa