Home » » Wawili mbaroni kwa tuhuma za kuwateka watoto

Wawili mbaroni kwa tuhuma za kuwateka watoto

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Polisi wa Kanda ya Dar es Salaam wamewakamata watu wawili wenye asili ya Kiasia ambao wanatuhumiwa kujihusisha na vitendo vya utekaji nyara.
Watu hao wanatuhumiwa kutaka kuwateka watoto wawili wa kike wa mfanyabiashara Aunally Jaffer anayeuza simu Mtaa wa Samora Dar es Salaam.
Kamanda wa kanda hiyo, Kamishna Suleiman Kova alisema walipata taarifa hizo Machi 14 mwaka huu na walipochunguza wakabaini kuna mpango ulioandaliwa na wafanyabiashara waliokuwa na lengo la kuwateka watoto hao, ili kujipatia Sh5 milioni kutoka kwa wazazi, ndugu na jamaa zao.
Alisema watoto waliolengwa kutekwa na watuhumiwa hao ni Shamima Aunally na Halifa Aunally wote ni wakazi wa eneo la Kisutu na Zanaki.
“Watuhumiwa walioandaa mpango huo ni mfanyabiashara mkazi wa Kariakoo, Adil Yusuf na mkazi wa Mtaa wa Jamhuri, Mehul Kava,” alisema Kamanda Kova.
“Walikamatwa wakiwa tayari kuwachukua mabinti hao ili waondoke nao, lakini polisi walishaweka mtego na kuwakamata eneo la Jet kabla ya kutimiza azma yao.”
Kamanda Kova alisema walipohojiwa walikiri kuwa lengo lao lilikuwa kujipatia fedha kupitia utekaji nyara huo.
Alisema uchunguzi unaendelea na jalada lipo kwa Mwanasheria wa Serikali, ili kuthibitisha mashtaka dhidi yao kabla ya kufikishwa mahakamani.
Alisema kwa sasa wasichana hao na familia yao wapo salama na wanashukuru kwa ushirikiano uliofanikisha kukamatwa kwao.
Chanzo;Mwananchi

0 comments:

 
Supported byBlogs za Mikoa
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa