Home » » WALIONUNUA IPTL WATOA NENO

WALIONUNUA IPTL WATOA NENO

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Katibu na Mshauri Mkuu wa Sheria wa Kampuni ya Kufua Umeme ya Independent Power Tanzania Ltd (IPTL) na Pan Africa Power Solutions (T) Ltd, Joseph Mwakandege akizungumza na waandishi wa habari kuhusu sakata la ununuzi wa IPTL. Kushoto ni Mwenyekiti Mtendaji wa Kampuni ya IPTL na PAP, Harbinder Singh Sethi

Wiki iliyopita gazeti hili liliandika kwamba fedha hizo zilitolewa baada ya Serikali kuamua kumaliza shauri hilo na hapo ndipo fedha hizo zilipochukuliwa katika akaunti hiyo na PAP.
Hata hivyo, pamoja na Seth kukubali kuchukua fedha hizo, alisema fedha zilizokuwamo ni Sh150 bilioni, huku akitetea hatua hiyo na ununuzi wa IPTL kwamba siyo kinyume cha sheria.
Kabla ya kuuzwa kwa PAP, IPTL ilikuwa inamilikiwa kwa ubia kati ya Mechmar Corporation ya Malaysia (asilimia 70) na VIP Engineering and Marketing Company Limited ya Tanzania iliyokuwa na asilimia 30.
PAP ni kampuni ya tatu katika mgogoro huo kujitokeza na kutoa ufafanuzi tangu habari zake zilipoanza kuandikwa. Kampuni ya kwanza ilikuwa ni VIP Engineering ya James Rugemalira na baadaye akaibuka Mwanasheria wa IPTL na wote walitetea mauzo hayo.
PAP ilivyonunua IPTL
Wakili wa PAP, Joseph Mwakandege alisema, kwa miaka mitano ya ITPL iliendeshwa bila kuwapo kwa mgogoro, lakini baadaye iliibuka mivutano miongoni mwa wanahisailiyosababisha kufunguliwa kwa akaunti ya Escrow.
Mwakandege alisema 2010, Sethi aliwasilisha nyaraka mahakamani kuonyesha kwamba alipewa mamlaka ya kusimamia mali zote za Mechmar hapa nchini.
Alisema, baadaye Sethi alinunua hisa zote ambazo awali Mechmar alikuwa ameuza kwa Piperlink na kuzihamishia PAP.
Kwa mujibu wa wakili huyo, Sethi baadaye alinunua asilimia 30 zilizosalia, na tayari mmiliki wa VIP, Rugemalira amekwishakiri kupokea Dola za Marekani 75 milioni (Sh120 bilioni) alizoziita kuwa ni fedha za ugoro.
Alisema baada ya mauzo hayo, VIP ilikwenda mahakamani na kuomba kesi zote zinazohusu kampuni hiyo na Mechmar zifutwe.
Septemba 5, mwaka jana, mahakama iliamua kufuta kesi hizo, hivyo PAP akapata haki ya kumiliki mali zote za IPTL, ikiwa ni pamoja na fedha zilizokuwa katika akaunti ya Escrow.
Mwakandege alisema baada ya uamuzi huo, PAP ilikubali kulipa madeni yote ya IPTL na ufilisi wa muda uliokuwa umewekwa kwa kampuni hiyo uliondolewa.
“Kutokana na hali hiyo, ilibidi kusainiwa mkataba kati ya IPTL na Serikali kupitia Wizara ya Nishati na Madini…Ifahamike kwamba akaunti ya Escrow ilikuwa mali ya wanahisa wa IPTL, haikuwa na fedha za walipakodi wala fedha za Benki ya Standard Chartered ya Hong Kong (mkopeshaji wa IPTL),” alisema Mwakandege.
Alifafanua kuwa, Serikali iliitaka PAP kusaini makubaliano kwamba iwapo watatokea wadai wapya wa IPTL itawalipa. Alisema baada ya hapo Serikali iliandika barua kwa BoT kuitaka iruhusu fedha hizo zilipwe kwa PAP.
Chanzo:Mwananchi

0 comments:

 
Supported byBlogs za Mikoa
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa