Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com
Home » » Kupinga utumikishwaji wa watoto si jukumu la serikali pekee

Kupinga utumikishwaji wa watoto si jukumu la serikali pekee


Benjamin Sawe-Maelezo.
Utumikishwaji wa watoto umekuwa ni tatizo kubwa duniani ambapo kutokana na tawkimu za makadirio za mwaka 2000-2012 za Shirika la Kazi Duniani asilimia 11 (watoto milioni 264) ya watoto wote duniani wenye umri wa miaka 5-17 wnatumikisahwa kwenye ajira za aina mbalimbali sawa na asilimia 11 ya watoto wenye umri huo.
Kwa upande wa Tanzania, utumikishwaji wa watoto kwa mwaka 2014/15 matokeo ya utafiti yanaonesha kuwa kati ya watoto milioni 15 wenye umri kati ya miaka 5 hadi 17 (watoto milioni 4.2) sawa na asilimia 28.8 wanatumikishwa katika kazi mbalimbali
Takwimu hizo zinaonesha kuwa sekta za kilimo na uvuvi zimeendelea kuwa sekta zinazoajiri watoto wengi zaidi ikiwa ni kiwango cha asilimia 92.1 ya watoto wote wanaojihusisha na shughuli za kiuchumi na wengi wao wanaishi vijijini.
Akizungumza katika uzinduzi wa ripoti ya matokeo ya utafiti wa utumikishwaji wa watoto Tanzania Bara wa mwaka 2014, Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu Dkt. Albina Chuwa anasema matokeo ya utafiti huo yanaonesha kuwa watoto hutumia zaidi ya nusu ya muda wao wa siku ikiwa ni asilimia 58.8 kwa shughuli za kujihudumia na usafi huku wasichana wakionekana kutumia muda mrefu zaidi kwa shughuli hizo kwa kiwango cha asilimia 58.3.
Ripoti hiyo inaendelea kuonesha shughuli za kujisomea kwa watoto zilichukua nafasi ya pili kwa matumizi ya muda kwa kiwango cha asilimia 15.5 ambapo wavulana wanatumia muda mrefu zaidi kwa shughuli za kujisomea ikiwani sawa ana asilimia 16.4 ikilinganishwa na wasichana waliotumia wastani wa asilimia 14.6
Dkt Chuwa anasema matokea hayo yakilinganishwa na nchi nyingine za Afrika kama Ghana yanaonesha kuwa watoto wa Kighana wenye umri wa miaka 10 hadi 17 wanatumia muda mwingi (asilimia 60.9) kwa siku kwenye shughuli za kujihudumia, usafi binafsi na starehe kama kuangalia runinga ikilinganishwa na asilimia 23.4 ya muda wao kwa siku kwenye shughuli za kujisomea.
Akizindua ripoti ya matokeo ya utafiti wa utumikishwaji wa watoto Tanzania Bara wa mwaka 2014, Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Watu wenye ulemavu Mh. Dkt. Abdallah Possi (Mb) anasema Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imesharidhia mikataba mbalimbali ikiwemo ya kikanda na kimataifa inayohusiana na ustawi na haki za watoto
Dkt. Possi anasema mikataba iliyoridhiwa ni pamoja na Mkataba Na. 138 wa Shirika la Kazi Duniani unaohusu umri wa chini unaoruhusiwa kujihusisha na ajira ya mwaka 1998 ambapo Mkataba na 182 wa utumikiswhaji wa watoto katika kazi hatarishi wa mwaka 2002 unatafsiri mtoto kama mtu mwenye umri chini ya miaka 18.
Aidha Tanzania imeridhia Mkataba wa Umoja wa Mataifa wa mwaka 1989 unaohusu Haki za Mtoto mwaka 1991, pia Serikali ilitunga Sheria ya Ajira na Mahusiano ya Kazi Na. 6 ya mwaka 2014 inayozuia kuajiri watoto wenye chini ya miaka 14 ambapo sheria hiyo inapiga marufuku kumfanyisha kazi mtot kwenye mazingira hatarishi yanayoweza kuidhuru afya yake.
Kwa mujibu wa Shirika la Kazi Duniani, utumikishwaji wa watoto unatafsiriwa kama ushiriki wa watoto katika kazi zinazomnyima mtot haki yake ya utoto, utu na fursa ya kujiendeleza ambazo pia huathiri watoto kiafya, kiakili, kielimu na kijamii.
Kama ilivyobainishwa katika Mkataba Na. 138 wa Shirika la Kazi Duniani, umri wa chini wa mtoto kujihusisha na ajira ni miaka 15 au 14 kutokana na muundo wa elimu ya msingi ya nchi husika
Kwa mujibu wa Ripoti ya Shirika la Kazi Duniani (ILO) kuhusu makadirio ya mwenendo wa utumikishwaji wa watoto duniani ya mwaka 2000-2012 inaonesha karibu nusu ya watoto wote wanaotumikishwa kwenye kazi mbalimbali, watoto milioni 85 wanatumikishwa kwenye kazi hatarishi (Hazodous Works) ambazo zinaathiri afya zao, usalama pamoja na makuzi yao.
Kutokana na tafiti hiyo utumikishwaji wa watoto wa mwaka 2014 Tanzania Bara umebaini kuwa, kuna idadi ya watoto milioni 15 wenye umri kati ya miaka 5-17 ambapo kati yao wavulana ni milioni 8 na wasichana ni milioni 7 na kundi kubwa la watoto ni wenye umri wa miaka 5-11 wakiwa ni asilimia 59.6 ya watoto wote ikifuatiwa na watoto wenye umri wa miaka 14-17 ambao ni asilimia 24.6.
Mgawanyo wa kijinsia wa watoto wanaojihususha na ajira kwenye sekta ya kilimo unaonesha kuwa wavulana ni asilimia 94.3 ya wavulana wote na wasichana ni asilimia 89.6 ya wasichana wote.
“Utumikishwaji wa watoto umekuwa ni tatizo kubwa duniani ambapo nchi mbalimbali ikiwemo Tanzania zinafanya jitiada za kutokomeza tazizo hili”Anasema Dtk. Possi.
Aidha matokeo ya utafiti wa utumikishwaji wa watoto wa mwaka 2014 yanabainisha kuwa kati ya watoto milioni 15 wenye umri kati ya miaka 5-17, watoto milioni 4.2, sawa na asilimia 28.8 wanatumikishwa katika kazi mbalimbali za kiuchumi hapa nchini.
Hata hivyo mwenendo wa utumikishwaji wa watoto umepungua kutoka asilimia 31.1 mwaka 2006 adi asilimia 28.8 mwaka 2014.
Kutokana na takwimu utafiti huo matokeo yanaonesha kuwa hali ya utumikishwaji wa watoto imekuwa ikiongezeka kadri umri unavyoongezeka ambapo watoto wenye umri wa kati ya miaka 14 hadi 17 wameonesha kuwa na kiwango cha juu cha asilimia 40.7 ikifuatiwa na watoto wenye umri wa miaka 12-13 sawa na asilimia 36.0 na miaka 5-11 sawa na asilimia 22.1
Kwa mgawanyiko wa kijiografia, matokeo yanaonesha kuwa tatizo la utumikishwaji wa watoto ni kubwa zaidi katika maeneo ya vijijini kwa asilimia 35.6 ikilinganishwa na maeneo ya miji mingine kwa asilimia 18.0 na Dar es Salaam kwa asilimia 3.6.
Utafiti huo unebainisha kuwa jumla ya watoto milioni 10.2 wenye umri wa miaka 5 hadi 17 wanahudhuria masomo shuleni, miongoni mwao wavulana ni milioni 5.2 sawa na asilimia 50.9 na wasichana ni asilimia 5.0 sawa na asilimia 49.1
Akizungumza hivi karibunu katika uzinduzi wa ripoti hiyo Dtk Possi anasema Serikali itaendelea kupambana vikali na kupinga utumikishwaji wa watoto nchini na kuhakikisha kuwa kiwango cha asilimia 28.8 kinapungua kwa kiasi kikubwa.
Dtk Possi anasema moja ya jitihada zilizofanywa na Serikali ya Awamu ya Tano kupambana na utumikishwaji wa watoto ni kuanzisha programu ya ELIMU BURE ili kuhamasisha mahudhurio ya watoto shuleni na kupunguza uwezekano wa watoto kujihusisha na ajira za utotoni.
“Natoa wito kwa wazazi na walezi kutumia vyema fursa ya kuwapeleka watoto shule ili kuwaondoa katika janga la utumikishwaji wa kuzuia mimba za utotoni
Aidha anawaomba Shirika la Kazi Duniani (ILO) kuendelea kushirikiana na Ofisi ya Taifa ya Takwimu kufanya uchambuzi zaidi wa kitaaluma ili kupata makadirio ya viwango vya utumikishwaji wa watoto katika ngazi za chini kama vile mkoa ili kudumusha hali halisi ya utumikishwaji wa watoto katika maeneo hayo.
MWISHO.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa