Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com
Home » » ORODHA YA MAHAKIMU NA MAJAJI WALIOVURUGA KESI ZA WAUZA UNGA KUTUA KWA JAJI MKUU

ORODHA YA MAHAKIMU NA MAJAJI WALIOVURUGA KESI ZA WAUZA UNGA KUTUA KWA JAJI MKUU

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Kamishina wa Mamlaka ya Kudhibiti Dawa za Kulevya nchini Rogers Sianga 

Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii.
JAJI Mkuu anatarajia  kupokea  orodha ya  majina ya mahakimu na majaji  ambao wamevuga kesi za watu wanaotuhumiwa kujihusisha na dawa za kulevya.

Hayo ameyasema leo  Kamishina wa Mamlaka ya Kudhibiti Dawa za Kulevya nchini Rogers Sianga wakati wa mkuatano wa viongozi mbalimbali wa kitaifa na waandishi wa habari ulioandaliwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda  kwa ajili  kupambana na dawa za kulevya.

 Sianga amesema kuwa kesi zimevurugwa na mahakimu na majaji. hivyo wale wote wanaohusika watashitakiwa na hata wawe na mali ambazo wamezipata kwa biashara hiyo zitataifishwa.

Amesema kuwa watazunguka katika maeneo mbalmbali ya jiji la Dar es Salaam ili kuhakikisha mtandao huo unapatikana na kwenda hata Zanzibar na mbinu zote wanazijua katika kufanya biashara hiyo.

Nae Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amemkabidhi orodha ya majina 97 wanaojihusisha na dawa za kulevya na kuongeza kuwa moto umewashwa dhidi ya watu wanaojihusisha na dawa za kulevya.

Amesema kuwa kuna nyumba 200 zinajihisisha na kufanya biashara ya madawa ya kulevya hapa jijini ambapo wote hao watafikiwa katika operesheni.

Nae Mohamed Khalid TID , amesema kuwa sasa ni mnyama ambae yuko tayari kupambana nawatu wanaouza pamoja na kutumia dawa za kulevya na amerudi kwa kufanya kazi na kuongeza kuwa kuimba hakuitaji dawa za kulevya.

Katika mkutano huo watu wawili wametakiwa kufika katika Kituo cha Polisi kati ambao ni Chidi Mapenzi,  Ayuob Mfaume Kiboko.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa