Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com
Home » » TAASISI YA MOYO JAKAYA KIKWETE (JKCI) KWA KUSHIRIKIANA NA TAASISI YA MADAKTARI AFRIKA YA NCHINI MAREKANI YAFANYA MATIBABU YA MOYO KWA WAGONJWA KWA KUWEKA KIFAA MAALUM CHA KUREKEBISHA MAPIGO YA MOYO ILI YAWE SAWA (KWA JINA LA KITAALAMU PACEMAKER)

TAASISI YA MOYO JAKAYA KIKWETE (JKCI) KWA KUSHIRIKIANA NA TAASISI YA MADAKTARI AFRIKA YA NCHINI MAREKANI YAFANYA MATIBABU YA MOYO KWA WAGONJWA KWA KUWEKA KIFAA MAALUM CHA KUREKEBISHA MAPIGO YA MOYO ILI YAWE SAWA (KWA JINA LA KITAALAMU PACEMAKER)

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

 Daktari Bingwa wa magonjwa ya Moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Peter Kisenge akizungumza na waandishi wa Habari kuhusu kambi maalum ya matibabu ya Moyo inayofanywa na Taasisi hiyo kwa kushirikiana na Taasisi ya Madaktari Afrika ya nchini Marekani kwa wagonjwa ambao mapigo yao ya moyo yako chini sana na hivyo kuwekewa kifaa maalum cha kurekebisha mapigo ili yawe sawa (kwa jina la kitaalamu Pacemaker) . Kushoto ni Daktari Bingwa na Magonjwa ya Moyo Mathew Sackett. Tangu kuanza kwa kambi hiyo mwanzoni wa juma hili jumla ya wagonjwa 20 wameshapatiwa matibabu kati ya hao nane wamewekewa Pacemaker na wengine wanne wanatarajia kuwekewa leo na kesho. 
 Daktari Bingwa wa magonjwa ya Moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Peter Kisenge akiwaonyesha waandishi wa Habari jina la Dkt. Mathew Sackett wa Taasisi ya Madaktari Afrika ya Nchini Marekani lilivyoandika katika nguo yake wakati wa mkutano baina yao uliozungumzia kambi maalum ya matibabu ya Moyo inayoendelea katika Taasisi hiyo kwa wagonjwa ambao mapigo yao ya moyo yako chini sana na hivyo kuwekewa kifaa maalum cha kuyarekebisha ili yawe sawa (kwa jina la kitaalamu Pacemaker) .
Daktari Bingwa wa magonjwa ya Moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Tulizo Shemu na mwenzake kutoka Taasisi ya Madaktari Afrika ya Nchini Marekani Mathew Sackett wakimwekea mgonjwa kifaa maalum cha kurekebisha mapigo ya moyo ili yawe sawa (kwa jina la kitaalamu Pacemaker) kifaa hicho huwekewa wagonjwa ambao mapigo yao ya moyo yako chini sana. Tangu kuanza kwa kambi maalum ya matibabu ya moyo jumla ya wagonjwa nane wameshawekewa Pacemaker na wengine wanne wanatarajia kuwekewa leo na kesho. 
 
  Wataalamu wa Magonjwa ya Moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na wenzao wa Taasisi ya Madaktari Afrika ya Nchini Marekani wakimwekea mgonjwa kifaa maalum cha kurekebisha mapigo ya moyo ili yawe sawa (kwa jina lakitaalamu Pacemaker) kifaa hicho huwekewa wagonjwa ambao mapigo yao ya moyo yako chini sana.
 

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa