Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com
Home » » UJENZI KAWE WAANZA TENA

UJENZI KAWE WAANZA TENA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.


Imeandikwa na Fransisca Emmanuel 

Mkurugenzi wa NHC, Nehemiah Mchechu
MRADI mkubwa wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), uliopo Kawe Dar es Salaam ambao ulisimama kwa mwaka mmoja kutokana na sababu mbalimbali, umeanza kazi na kwamba unalenga kufanya eneo hilo kuwa Kitovu cha Biashara jijini humo.
Akizungumza wakati wa ziara iliyofanywa na Kamati ya Mipango miji na Mazingira Manispaa ya Kinondoni, Mkurugenzi wa NHC, Nehemiah Mchechu, alisema mradi huo unatarajiwa kukamilika kati ya mwaka 2019 na 2020 ambao unagharimu zaidi ya dola za kimarekani bilioni mbili.
Mchechu alisema sababu za kusimama kwa mradi huo walikuwa wanasubiri kujiridhisha namna ya uendeshaji wa mradi huo ikiwemo gharama zote pamoja na kupata kibali kutoka Wizara ya Fedha.
“Mradi huu unaojulikana kama 711, utawanufaisha watu zaidi ya 50,000 kwa kuwa utakuwa na biashara kwa saa 20,’’ alisema. Pia alisema wanategemea mradi huo utaleta maendeleo kwa miaka 50 ijayo kwa kuwa licha ya kuwepo kwa makazi 262, watajenga miundombinu ya usafiri.
CHANZO HABARI LEO

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa