Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com
Home » » Serikali yatoa Msimamo wake kwa Klabu ya Simba kuhusu suala la uwekezaji

Serikali yatoa Msimamo wake kwa Klabu ya Simba kuhusu suala la uwekezaji

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe akieleza waandishi wa habari (hawapo pichani) msimamo wa serikali kwa Klabu ya Michezo ya Simba kuhusu suala la uwekezaji kwa vyama vya michezo vilivyoanzishwa na wanachama kwa kuzingatia wa sheria kuwa ni 49% kwa mwekezaji na 51% kwa wanachama kufuatia kutangaza kumpa mwekezaji wao 50% hivi karibuni kinyume na kanuni jana jijini Dar es Salaam,Kushoto ni Kaimu Rais wa Klabu ya Michezo ya Simba Bw.Salim Abdallah na Katikati ni Katibu Mtendaji Baraza la Michezo la Taifa Bw. Mohamed Kiganja.
Kaimu Rais wa Klabu ya Michezo ya Simba Bw. Salim Abdallah akieleza waandishi habari (hawapo pichani) kuwa msimamo wa serikali wameuelewa na watakwenda kuzungumza na mwekezaji wao Mohamed Dewji kuhusu kumpunguzia 1% na kumpa 49% badala ya 50% waliyokuwa wametangaza hivi karibuni kumpa jana jijini Dar es Salaam,pembeni yake ni Mwanasheria wa Klabu ya Michezo ya Simba Bw.Evodius Mtawala.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa