Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com
Home » » KAIMU KATIBU MKUU WA MAMBO YA NJE AKUTANA KWA MAZUNGUMZO NA MBUNGE KUTOKA UTURUKI

KAIMU KATIBU MKUU WA MAMBO YA NJE AKUTANA KWA MAZUNGUMZO NA MBUNGE KUTOKA UTURUKI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushiriano wa Afrika Mashariki, Balozi Ramadhan M. Mwinyi akiwa katika mazungumzo na Mhe. Zehra Taskesenlioglu, Mbunge na Mwenyekiti wa Umoja wa Wabunge wa Bunge la Uturuki wanaounda Kundi la Wabunge Marafiki na Wabunge wa Bunge la Tanzania alipofika Wizarani tarehe 23 Februari, 2018. Katika mazungumzo yao walizungumzia umuhimu wa kukuza na kuimarisha mahusiano kati ya Tanzania na Uturuki katika nyanja mbalimbali ikiwemo elimu.
Balozi wa Uturuki nchini, Mhe. Ali Davutoglu (kulia) akiwa pamoja na Bw. Aytak Dincer, Mwekezaji na Mwenyekiti wa Baraza la Biashara la Tanzania na Uturuki wakifuatilia mazungumzo kati ya Balozi Mwinyi na Mhe. Zehra (hawapo pichani)
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Salvator Mbilinyi (kulia) akiwa na Bw. Hassan Mwamweta, Afisa Mambo ya Nje wakifuatilia mazungumzo
Kikao kikiendelea

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa